Mpesa Safaricom- Vodacom,

acha upumba bana, hizi ni hela nilikuwa namrejeshea rafiki yangu alikuwa ananidai
pole bro. kufatilia hizo pesa zitakupotezea mda mwingi na pesa zaidi. chukulia ni kama umepeana sadaka na usahau
 
Taratibu za usajili zinafanana, hata Tz huwezi kusajili line ya simu kienyeji. Kwa kifupi huyo aliyepokea pesa anaweza kupatikana kirahisi sana
 
nafikiria sana ili jambo la "instant money" tunabidi tuliangazie tena, voda/safcom wanabidi wafikirie sana....maoni yangu lakini.
Mwambie yule uliyekuwa unamtumia akamshitaki mpokeaji kwa niaba yako, nawe utatakiwa kutoa ushahidi
 
Ni tshilingi ngapi?, tuanzie hapo kwanza, lengo ni kulinganisha na ghalama ya kumpata mwizi wako na kiasi ulichopoteza ili tuona kama kuna haja ya kufanya hivyo.
 
Kwani nyie mpesa yenu haiwapei jina la unakotuma, to confirm before hujatuma.
Mkuu ndivyo ilivyo kwa voda unapotuma pesa Kenya hawakupi jina hadi utume
 
pole bro. kufatilia hizo pesa zitakupotezea mda mwingi na pesa zaidi. chukulia ni kama umepeana sadaka na usahau
ata ndivyo nimefikiria, nimeachana nazo , hali ya maisha.
 
Mwambie yule uliyekuwa unamtumia akamshitaki mpokeaji kwa niaba yako, nawe utatakiwa kutoa ushahidi
voda wanasema ivyo, ila nimeona acha tu niachane nazo tu manake sitaki kumsumbua rafiki yangu tayari hana furaha nime mess tayari na vibaya zaidi ni kumpa kazi ya ziada.
 
Weka namba yake hapa tukusaidie kumtafuta akuludishie hela zako. Sio poa kabisa alivyofanya maisha ni magumu kwa wote.
 
Unapaswa kutoa malalamiko kwa vodacom, na ukimshitaki polisi atapatikana kirahisi tu
Ata wakimpata ata sema na mimi nilikua nategemea pesa kuingia so ilivyo ingia nikajua ndiyo hiyo nikaitumia!
 
Duh! Pole, ila kwa hela hamna lingine zaidi ya kuwa makini tu, siku hizi Bongo hata ukipiga simu hairudishwi kiulaini, maana kuna matapeli walikua wamezoea, kwa mfano mtu anaishi hotelini halafu wakati anatoka anawalipa kwa Mpesa, akiwa nje na mbali anapiga simu Voda kwamba kakosea wanamrejeshea.

Mimi huwa natuma sana na kupokea hela kutoka Bongo kwa njia ya Safaricom-Voda lakini huwa makini herufi kwa herufi, naitaja kwa sauti, au natumia copy pasting.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…