Pre GE2025 Mpina alikuwa sahihi kuagiza sukari nje ni kupoteza fedha za kigeni

Pre GE2025 Mpina alikuwa sahihi kuagiza sukari nje ni kupoteza fedha za kigeni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwa kumbukumbu zangu, katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, Mhe. Mpina alisema kuagiza sukari nje ni kupoteza fedha za kigeni.

Jana tarehe 04/08/2024, Mama Samia anaripotiwa kukirii japo hakunyoosha maelezo kuwa tunapoteza fedha za kigeni ambazo tungeweza kuzitumia kwa mambo mengine na pia ingesaidia ku-control tatizo la fedha za kigeni hapa nchini.

Naona watu wamesahau kuhusu hili na Lucas Mwashambwa nae sijui kasahau au anajisahaulisha.

Hakika muda ni hakimu wa haki.

PIA SOMA
- Mpina kuwapeleka Mahakamani Waziri Bashe na Bodi ya Sukari kwa kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha Sheria

1722869339324.png
 
Kwa kumbukumbu zangu, katika taarifa yake kwa waandishi wa habari, Mhe. Mpina alisema kuagiza sukari nje ni kupoteza fedha za kigeni.

Jana tarehe 04/08/2024, Mama Samia anaripotiwa kukirii japo hakunyoosha maelezo kuwa tunapoteza fedha za kigeni ambazo tungeweza kuzitumia kwa mambo mengine na pia ingesaidia ku-control tatizo la fedha za kigeni hapa nchini.

Naona watu wamesahau kuhusu hili na Lucas Mwashambwa nae sijui kasahau au anajisahaulisha.

Hakika muda ni hakimu wa haki.

PIA SOMA
- Mpina kuwapeleka Mahakamani Waziri Bashe na Bodi ya Sukari kwa kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha Sheria

Speaker hapo tumbo joto na ninadhani atakuwa mbunge wa bunge moja na usipika wa awamu moja. Dkt Samia keshagundua hamsaidii kabisa ktk muhimili wake zaidi ya kuruhusu Dkt Samia kudhalilishwa kwa kuonekana mzembe. Suala kama hili la sukari ni la kimfumo wala halihitaji rais kuingilia kati kabisa, kama mfumo wa bunge ungefanya kazi leo hao wahuni wangekuwa wameshawajibishwa.
 
Bora wameanza kuona hili. Bidhaa nyingi sana zinatupotezea pesa za kigeni. Kuna takataka nyingi sana za Kichina. Kuna mafuta ya kula, ngano, nk nk. Tukipanga mambo yetu vizuri tutaongeza pesa za kigeni.
Hapo kwenye ngano kuna shida sana. Kuna uwezekano mkubwa wa kuzalisha ngano humu humu nchini.
Mafuta mengi ni ya mawese kutoka Asia. Bora Mzee Magufuli alisisitiza Kilimo cha michikichi Kigoma, kuanzisha mashamba ya Magereza n.k akilenga kupunguza importation
 
Back
Top Bottom