Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina ameuliza swali bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza adhabu ya kutohudhuria vikao 15 vya Bunge, akitaka kufahamu mkakati wa haraka wa serikali katika kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma za matibabu kwa kujenga na kumalizia zahanati ambazo wananchi walishajitolea kwa nguvu kazi.
Akijibu swali hilo kwa niaba ya Ofisi ya Rais TAMISEMI (Afya), Naibu Waziri Dkt. Festo Dugange ameeleza kuwa vijiji vyote vyenye sifa ya kujengewa zahanati vinaendelea kujengewa, na pia mitaa yote yenye sifa inajengewa zahanati kwa lengo la kuboresha huduma za afya vijijini.
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina ameuliza swali bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza adhabu ya kutohudhuria vikao 15 vya Bunge, akitaka kufahamu mkakati wa haraka wa serikali katika kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma za matibabu kwa kujenga na kumalizia zahanati ambazo wananchi walishajitolea kwa nguvu kazi.
Akijibu swali hilo kwa niaba ya Ofisi ya Rais TAMISEMI (Afya), Naibu Waziri Dkt. Festo Dugange ameeleza kuwa vijiji vyote vyenye sifa ya kujengewa zahanati vinaendelea kujengewa, na pia mitaa yote yenye sifa inajengewa zahanati kwa lengo la kuboresha huduma za afya vijijini.