Mpoki ni mchekeshaji mzuri na kwa kweli ana kipaji au karama ya kazi hiyo.
Ametuchekesha na kuyuelimisha muda mrefu na jina lake lilivuma zaidi wakiwa original comedy pale EA Radio na kubwa lao tbc.
Hivi sasa yupo EFM RADIO na kazi yake ya kuchekesha nasema bado ni superb. Lakini siku hizi wakati mwingine anavuka mstari kutoka kuchekesha hadi kukejeli na hata kutukana watu kwa hali zao, kipato chao, kazi zao, umasikini wao na hata maumbo yao!
Mpoki anakejeli wanaoishi nyumba za kupanga. Kisa sijui yeye ana mjengo. Akumbuke aliyempa yeye ndiye aliyewanyima hao wenye miaka 50 na hawana nyumba.
Si wote wasio na nyumba hadi wanzeeka ni kwa sababu ya ujinga au uzembe wao. Miscalculations may be lakini Mpoki hawasaidii kwa kuwakejeli. Mujuni ajue hao anaowadharau leo ndio waliompa umaarufu.
Mujuni si vizuri kuwakejeli wauza kahawa, maji, mitumba au vitumbua. Haiewezekani wote wakatoka kupitia comedy.
Acha kuwatukana wasio na magari au wenye magari vimeo. Wenye samani mbaya kwenye nyumba zao. Acha majivuno bwana wenye vitambi na hawana nyumba au magari nao wana haki ya kuishi, kupanda daladala nk.
Mpoki aka Mujuni una akili sana. Huwa nakufuatilia unavyojenga hoja katika kipindi cha ubaoni. Wewe ni kichwa. Ila nasema usilewe umaarufu. Acha kusanifu watu. Kuna tofauti kati ya kuwachekesha watu na kuwakejeli/tukana. Kila la kheri Mujuni. Sisi marafiki wako wa mbali tunaona anapokosea na tunakwambia. Marafiki zako wa karibu hawawezi kukwambia hata ukosee kiasi gani. All da best Mpoki aka mwarabu wa Dubai.
Ametuchekesha na kuyuelimisha muda mrefu na jina lake lilivuma zaidi wakiwa original comedy pale EA Radio na kubwa lao tbc.
Hivi sasa yupo EFM RADIO na kazi yake ya kuchekesha nasema bado ni superb. Lakini siku hizi wakati mwingine anavuka mstari kutoka kuchekesha hadi kukejeli na hata kutukana watu kwa hali zao, kipato chao, kazi zao, umasikini wao na hata maumbo yao!
Mpoki anakejeli wanaoishi nyumba za kupanga. Kisa sijui yeye ana mjengo. Akumbuke aliyempa yeye ndiye aliyewanyima hao wenye miaka 50 na hawana nyumba.
Si wote wasio na nyumba hadi wanzeeka ni kwa sababu ya ujinga au uzembe wao. Miscalculations may be lakini Mpoki hawasaidii kwa kuwakejeli. Mujuni ajue hao anaowadharau leo ndio waliompa umaarufu.
Mujuni si vizuri kuwakejeli wauza kahawa, maji, mitumba au vitumbua. Haiewezekani wote wakatoka kupitia comedy.
Acha kuwatukana wasio na magari au wenye magari vimeo. Wenye samani mbaya kwenye nyumba zao. Acha majivuno bwana wenye vitambi na hawana nyumba au magari nao wana haki ya kuishi, kupanda daladala nk.
Mpoki aka Mujuni una akili sana. Huwa nakufuatilia unavyojenga hoja katika kipindi cha ubaoni. Wewe ni kichwa. Ila nasema usilewe umaarufu. Acha kusanifu watu. Kuna tofauti kati ya kuwachekesha watu na kuwakejeli/tukana. Kila la kheri Mujuni. Sisi marafiki wako wa mbali tunaona anapokosea na tunakwambia. Marafiki zako wa karibu hawawezi kukwambia hata ukosee kiasi gani. All da best Mpoki aka mwarabu wa Dubai.