Mr. Ebbo: Kilichomuua chajulikana?!?

Mr. Ebbo: Kilichomuua chajulikana?!?

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,131
Reaction score
937
KIFO CHA MR. EBBO... KILICHOMUUA CHAJULIKANA





Abel Loshilaa Motika a.k.a Mr Ebo enzi za uhai wake.

[h=3]KIFO CHA MR. EBBO... KILICHOMUUA CHAJULIKANA[/h]


ebbo2.jpg

Na Joseph Ngilisho, Arusha
VILIO, majozi na huzuni, bado vimelizunguka Jiji la Arusha kufuatia kifo cha staa mkubwa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo mwenye ladha ya asili ya kabila la Wamasai, Abel Loshilaa Motika a.k.a Mr Ebo (37), aliyefariki usiku wa kuamkia Ijumaa iliyopita, Desemba, Mosi mwaka huu.
NINI KIMEMUUA? Swali lililokuwa likizunguka, lilihoji ni nini kilichomuua Mr. Ebbo aliyekuwa amelazwa kwa muda katika Hospitali ya Mission iliyopo nje kidogo ya Jiji la Arusha, Usa River wilayani Arumeru angali bado akipendwa na mashabiki wake?
UPUNGUFU WA DAMU NI UGONJWA GANI? Kwa mujibu wa kaka wa marehemu aliyezungumza na The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda katika boma la Motika maeneo ya Masai Camp, Moshilaa Motika, mdogo wake alisumbuliwa na upungufu wa damu mwilini kwa muda mrefu. NI ANEMIA AU LEUKEMIA? Gazeti hili liliwadodosa madaktari bingwa juu ya hali hiyo kiafya ambapo magonjwa yanayosumbua wengi hivi sasa ya Anemia na Leukemia yalitajwa.



http://fredynjeje.blogspot.com/2011/12/kifo-cha-mr-ebbo-kilichomuua.html
CHANZO CHA IJUMAA WIKIENDA Kwa mujibu wa chanzo chetu, Mr. Ebbo amekuwa akisumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa huo ambapo alikuwa akiishiwa damu, lakini cha kushangaza, muda mfupi baada ya kuongezewa nyingine, bado hali ilibaki vilevile. DAMU ILIKUWA INAKWENDA WAPI? Chanzo hicho kilidai kuwa ilifika wakati hata madaktari wakawa wanashangaa damu inakwenda wapi kufuatia hali ya kuongezewa nyingine, lakini vipimo vikaonesha kama hajaongezewa chochote.


DAMU YAPELEKWA NJE YA NCHI Ilidaiwa kuwa katika harakati za kupigania uhai wa Mr. Ebbo aliyetamba na kibwagizo cha ‘Mi Mmasai Bana', madaktari walifikia hatua ya kupeleka damu yake nje ya nchi kwa ajili ya vipimo, lakini wataalam waligonga mwamba. AHAMISHIWA ARUSHA Habari zilizidi kudai kuwa baada ya hali kuzidi kuwa mbaya, alihamishiwa Arusha kwani baadhi ya ndugu walidhani kinachosababisha aumwe ni mazingira ya Jiji la Tanga alikokuwa akiishi na kuendesha shughuli zake ikiwemo studio yake ya muziki ya Motika Records.




Kaka yake marehemu.

Hata hivyo, pamoja na jitihada zote hizo ndani na nje ya nchi, Mr. Ebbo aliyekuwa amejipanga vilivyo kwenye gemu alitangulia mbele ya haki.ARUSHA YAZIZIMA Baada ya kutangazwa kwa kifo cha Mr. Ebbo ambaye ukiwa umekasirika na ukasikia wimbo wake lazima ucheke, Jiji la Arusha lilizizima kwa majonzi huku msanii huyo akikumbukwa zaidi kwa vichekesho vyake.
http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/kifo-cha-mr-ebbo-kilichomuua-chajulikana



Maelfu ya wakazi wa mji wa Arusha jana waliungana na wanafamilia wa Msanii Maarufu Mr Ebbo katika misa maalum ya kuuombea Mwili wa Marehemu motto wao na baade katika maziko yaliyofanyika mjini humo.




Familia ya marehemu Ebo katikati mama mzazi,kulia baba yake mzazi na kaka yake mkubwa Olais Motika wakiwa msibani hapo.

Ndugu mbalimbali wakiaga mwili wa marehemu.



Wazazi wa Mr Ebbo wakiwa na Mbunge wa Zamani na Waziri wa Mazingira, Dk. Batilda Buriani.

watoto watatu wa marehemu Mr Ebo ,wakifarijiwa na ndugu.



Naibu waziri wa Ardhi ,nyumba na makazi,Goodluck Ole Medeye kulia akimfariji baba mzazi wa marehemu Ebo,mzee Loshilaa Motika katika ibada ya mazishi ya marehemu Mr,Ebbo juzi nyumbani kwake Moshono ,katikati ni aliyewahi kuwa waziri wa mazingira dkt Batilda Burian.


Kaka mkubwa wa marehemu mr,Ebbo Olais Motika kushoto na mdogo wake wa mwisho Jackson Motika,wakiwa katika ibada ya mazishi ya marehemu,Mr Ebbo jana nyumbani kwao Moshoni jijini Arusha.



Maelfu ya wakazi wa mjini Arusha wakiwa katika foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho kwenye mwili wa Marehemu Mr Ebbo.
askofu1.jpg

askofu2.jpg

Maelfu ya wakazi wa mji wa Arusha jana waliungana na wanafamilia wa Msanii Maarufu Mr Ebbo katika misa maalum ya kuuombea Mwili wa Marehemu motto wao na baade katika maziko yaliyofanyika mjini humo.
Miongoni mwa viongozi walioshiriki mazishi hayo ni pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye ambaye ni Mbunge wa Arumeru Mashariki pamoja na Waziri wa Zamani wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Batilda Buriani na wasanii mbalimbali wa muziki nchini.
Mr Ebbo alifariki mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuugua kwa muda.
Askofu akiongoza misa ya kumuombea Marehemu Abel Loshilaa Motika "Mr Ebbo" nyumbani kwao mjini Arusha jana .
DSC06670.JPG

Familia ya marehemu Ebo katikati mama mzazi,kulia baba yake mzazi na kaka yake mkubwa Olais Motika wakiwa msibani hapo.

DSC06672.JPG

Ndugu mbalimbali wakiaga mwili wa marehemu.



Wazazi wa Mr Ebbo wakiwa na Mbunge wa Zamani na Waziri wa Mazingira, Dk. Batilda Buriani.
DSC06683.JPG

Watoto watatu wa marehemu Mr Ebo ,wakifarijiwa na ndugu.


DSC06695.JPG

Naibu waziri wa Ardhi ,nyumba na makazi,Goodluck Ole Medeye kulia akimfariji baba mzazi wa marehemu Ebo,mzee Loshilaa Motika katika ibada ya mazishi ya marehemu Mr,Ebbo juzi nyumbani kwake Moshono ,katikati ni aliyewahi kuwa waziri wa mazingira dkt Batilda Buriani.

DSC06700.JPG

Kaka mkubwa wa marehemu mr,Ebbo Olais Motika kushoto na mdogo wake wa mwisho Jackson Motika,wakiwa katika ibada ya mazishi ya marehemu,Mr Ebbo jana nyumbani kwao Moshoni jijini Arusha.

DSC06703.JPG

DSC06704.JPG

Maelfu ya wakazi wa mjini Arusha wakiwa katika foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho kwenye mwili wa Marehemu Mr Ebbo.



KUZIKWA LEO Mr. Ebbo atazikwa leo katika boma la Motika maeneo ya Masai Camp Moshono, nje kidogo ya Jiji la Arusha yakitanguliwa na misa maalumu ya kuuombea mwili wa merehemu katika Kanisa la Lutheran lililopo Kata ya Olorieni. HISTORIA Mr Ebbo alikuwa mtoto wa 10 kati ya watoto 11 wa mzee Loshilaa Motika (85), ambapo kati yao wawili ni marehemu akiwemo Mr. Ebbo ambaye ameacha mke na watoto watatu.KUTOKA IJUMAA WIKIENDA Mungu ametoa na Mungu ametwaa, jina lake lihimidiwe. Rest In Peace Mr. Ebbo!





Maelfu ya wakazi wa mji wa Arusha jana waliungana na wanafamilia wa Msanii Maarufu Mr Ebbo katika misa maalum ya kuuombea Mwili wa Marehemu motto wao na baade katika maziko yaliyofanyika mjini humo.


Miongoni mwa viongozi walioshiriki mazishi hayo ni pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye ambaye ni Mbunge wa Arumeru Mashariki pamoja na Waziri wa Zamani wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Batilda Buriani na wasanii mbalimbali wa muziki nchini.


Mr Ebbo alifariki mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuugua kwa muda.
Askofu akiongoza misa ya kumuombea Marehemu Abel Loshilaa Motika "Mr Ebbo" nyumbani kwao mjini Arusha jana .

Familia ya marehemu Ebo katikati mama mzazi,kulia baba yake mzazi na kaka yake mkubwa Olais Motika wakiwa msibani hapo.

Ndugu mbalimbali wakiaga mwili wa marehemu.



Wazazi wa Mr Ebbo wakiwa na Mbunge wa Zamani na Waziri wa Mazingira, Dk. Batilda Buriani.

watoto watatu wa marehemu Mr Ebo ,wakifarijiwa na ndugu.



Naibu waziri wa Ardhi ,nyumba na makazi,Goodluck Ole Medeye kulia akimfariji baba mzazi wa marehemu Ebo,mzee Loshilaa Motika katika ibada ya mazishi ya marehemu Mr,Ebbo juzi nyumbani kwake Moshono ,katikati ni aliyewahi kuwa waziri wa mazingira dkt Batilda Burian.


Kaka mkubwa wa marehemu mr,Ebbo Olais Motika kushoto na mdogo wake wa mwisho Jackson Motika,wakiwa katika ibada ya mazishi ya marehemu,Mr Ebbo jana nyumbani kwao Moshoni jijini Arusha.



Maelfu ya wakazi wa mjini Arusha wakiwa katika foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho kwenye mwili wa Marehemu Mr Ebbo.


Posted in:
 
mtaani yanasemwa mengi!ukijua gonjwa hili linatisha hamna anayethubutu kunyanyua mdomo wake na kusema anachosikia!ukweli utabaki palepale gonjwa hili lipo na linamaliza watu kila siku!tuache zinaa na kumuomba Mola atuepushe na maradhi!nayasema haya si kwa dhihaka ama la!nasema huku roho inaniuma na machozi yananitoka!lini watanzania tutakuwa wakweli!kuna mtangazaji ana fununu za gonjwa hili kila siku watu wanamnyooshea kidole je kutakuwa na mwenye ujasiri wa kumsema siku Mola akiamua kumchukua kiumbe wake?au watu wanafanya hayo kwa chuki naye?.........narudi!mtaani yanasemwa mengi kuhusu kifo cha Ebbo ila si wakati wa kujadili wafu!
 
Muuza sura naunga mkono hoja yako,ni kweli yanasemwa mengi kinyume na niliyosoma hapa,lkn mimi na wewe hatuna uhakika na zaidi sana hata kama uhakika ungekuwepo Tanzania hakuna ujasiri wa kuweka mambo wazi!! :coffee:
 
Muuza sura naunga mkono hoja yako,ni kweli yanasemwa mengi kinyume na niliyosoma hapa,lkn mimi na wewe hatuna uhakika na zaidi sana hata kama uhakika ungekuwepo Tanzania hakuna ujasiri wa kuweka mambo wazi!! :coffee:

Kuna wale wanaomuhusisha na maisha ya Dada aliyejipatia umaarufu katika miaka fulani hivi wa kimasai akiitwa NDUKAI wakati huo akiishi Kinos,..huyu nae hayupo tena kati yetu....R.I.P
 
Kuna wale wanaomuhusisha na maisha ya Dada aliyejipatia umaarufu katika miaka fulani hivi wa kimasai akiitwa NDUKAI wakati huo akiishi Kinos,..huyu nae hayupo tena kati yetu....R.I.P
Kinos ndo wapi?
R.I.P
 
ooh well i hope you have found peace huko....,sie bado tunaendelea na dunia yetu iliyojaa madhila. RIP
 
Hizi comment nane za leo kwenye hii thread ya miaka mingi iliyopita imenikumbusha siku niliyoisahau njia ninayoipita kila siku na kulazimika kuomba nielekezwe njia ya kuelekea home! Watu wakabaki wananishangaa! Maana barabara yenyewe ndiyo hiyo hiyo niliyoikanyaga!! PAGAN anauliza kama Mr Ebbo amekufa alhamisi hii kwenye thread ya mwaka 2011 inayohusu kifo cha Ebbo!!
 
Ameshaondoka haina maana tenaa kufatilia kilichomua
 
Back
Top Bottom