Mradi gani wa kiuchumi unaweza kuanzisha kwa kutumia fedha za mafao kiasi cha Tshs 90,000,000/-?

Econometrician

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2013
Posts
16,879
Reaction score
31,253
Wana JF habari zenu,

Mama yangu baada ya kunusurika na kikotoo ameniomba nimshauri kumpendekezea mradi ambao anaweza akaanzisha na kuusimamia yeye mwenyewe, pesa anazotegemea kupata ni Tshs. 94,000,000.

Fedha anayotegemea kuanzishia mradi ni tshs 90,000,000.

Nimeona ni vyema kuwashirikisha kupata mawazo mbadala, pkwa kuwa ninaamini baadhi yetu wazazi wetu walistaafu na kuanzisha miradi ambayo imekuwa imara na endelevu mpaka sasa.
 
Atafute mazingira mazuri atenge fedha kiasi ajikite kwenye ufugaji!
Anaweza kufuga ng'ombe wa maziwa kwa Iringa Lita 1000 Na unakuta asas anafuata mpaka njombe ko demand bado ni kubwa!
Halafu ni mradi ambao hauleti stress sana!
Akipata mbegu nzuri angalau ya kutoa Lita 10+ inalipa sana!

Lakini kama anaweza anaweza akajikita kwenye ufugaji wa kuku Mfano chotara mahitaji ya mayai bado ni makubwa halafu haihitaji kutumia nguvu sana kuhudumia kama ng'ombe wa maziwa, Kwahiyo hii ata hawa wastaafu wanaweza kufanya!

Ingawa sijui kama atakuelewa Maana wastaafu na kununua nyumba mjini ni kama paka Na maziwa!

NB; Hiyo miradi inahitaji usimamizi wa karibu sana wa mwenye mali mwenyewe asije akajiroga kufuga kwa remote (yupo dar mradi upo njombe) atalia
 
Najua mnaishi mjini sana..mwambie atafute eneo kubwa ajenge nyumba nyingine pembezeni kidogo ya mji ambayo mtahamia kuishi huko..iyo nyumba ya mjini aikarabati katika mfumo iwe nyumba ya kupangisha ikiwezekana ajenge na nyumba nyingine hapohapo mjini palipochangamka iwe ya kupangisha so jumla ya nyumba zenye wapangaji mtakuwa nazo mbili hapo kila mwezi atakuwa anapata kodi..huko mtakapohamia etenge eneo kubwa kwa ajili ya ufugaji ng'ombe na kuku ikiwezekana na mifugo mingine alafu atafute kijana kutoka kijijini kwa ajili ya kuhudumia iyo mifugo na ambae atakuwa anamsaidia kuuza hizo bidhaa zitokanazo na mifugo kama maziwa..mayai..etc...kwa kuwa mama umri umeenda kama kuna visenti kidogo vitabaki hapohapo nyumbani mtakapohamia aweke duka la bidhaa za nyumbani so hapo ndo itakuwa sehemu yake ya kupiga Story na kupata hela ndogondogo...ukifuata huu ushauri najua kuna siku utanitafuta unishukuru
 
Mradi wenye risk ndogo ni kujenga nyumba eneo zuri na kuipangisha kwa miaka mitano alafu unaiuza kwa faida,kama ni biashara kama unaweza kuingiza faida ya uhakika ya milioni moja na nusu kwa mwezi kwa mtaji wa milioni tisini siyo mbaya,wenye uzoefu na biashara watakwambia kwa mtaji huo ni faida ndogo lakini kumbuka ni bora kupata faida ndogo kuliko kurisk na kupoteza mtaji wote.
 
Anapoishi ni Vijijini,yes anapenda mradi ambao atasimamia mwenyewe ila kwa kufuga ni ngumu kidogo kwa kuwa hamna soko la maziwa wala wayai.
Pia alikuwa na lengo hilo la kununua nyumba mjini na kuipangish but binafsi yangu sikuona kama ni zuri sana.
 
Yani 90M yote muitupe kwenye mradi Loh! jina lako ni econometrician haujui au hautambui kwenye biashara kuna Profit and loss? Mtakula nyasi ohoooo
Mkuu kuwa mchumi sio kujua kila kitu,haya mambo ya uwekezaji yanahutaji ideas pia.
Pia hajapanga ku invest 90M mahali pamoja ndio maana nimeandika huu uzi kuomba ushauri
 
Ushauri umezingatiwa.
 
Anapoishi ni Vijijini,yes anapenda mradi ambao atasimamia mwenyewe ila kwa kufuga ni ngumu kidogo kwa kuwa hamna soko la maziwa wala wayai.
Pia alikuwa na lengo hilo la kununua nyumba mjini na kuipangish but binafsi yangu sikuona kama ni zuri sana.
Ni wazo zuri kwa upande wake hasa ukizingatia na umri wake kwasababu hana ile kimuhe muhe cha kutengeneza faida ya haraka Kwahiyo hata akiwa anakusanya laki 2 kwa mwezi isoooooke!

Halafu hiyo kwake ni ishu ambayo haitamstress zaidi ya kugombana na wapangaji wakorofi tu!
Kwahiyo ni jambo jema pia
 
Ndio Maana amekuja kuomba ushauri mkuu!
Halafu mbona hakuna mahali amesema kwenye biashara kuna faida tu !
Ni tahadhali tu mkuu nina ushuhuda wa Mwalimu wangu mmoja kastaafu 2016 alipata hiyohiyo 90M akawekeza vibaya mno kwenye kilimo cha vitunguu na matrekta pesa yote aliitia kule sasa hivi anatamani aajiriwe upya anafundisha kila amuonaye huko kijijini kwao Dish limeyumba
 
Kwa heshima ya mama yetu mstaafu naomba nimshauri kama ifuatavyo:

Achukue 50m aweke fixed diposit atapata pesa kidogo ya kula kwa kipindi cha mwaka mzima;

Anunue mashamba maeneo ya pwani kama hekari 12 na kuchimba kisima roughly kama 12m;

Apande miti ya korosho kwenye hekari 10 roughly itamgharimu kama 2m (itachukua miaka mitatu kukua awe na subra);

hekari mbili afuge kuku wa kienyeji na kupanda mboga na matikiti maji, mabanda, kuku, na mbegu za matikiti maji na labour inaweza ikamgharimu kama 3m;

Milion 27 iliyobaki afikirie kujenga kajumba cha kizushi huko shamba au anunue gari awe anaenda kuangalia shamba
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] vitunguu!
Alishawahi kula mkenge bro wangu nahisi hupendi ata kusikia kuhusu hicho kilimo cha vitunguu
 
Kama kuna biashara alikuwa anafanya kwa kiasi cha kujua abc ya hiyo biashara, sasa anaweza kuanza kuongeza mtaji kidogo kidogo. Mfano kama biashara ya sasa ina thamani ua mil 10, ongezo la mtaji ghafi inaweza kuwa 5m ili aendelee kuweza kuimudu.

Kama hajawahi kufanya boashara yeyote ile, risk ya kuanza na 90m ni kubwa mno. Ni vizuri aanza na mradi utakaotumia mpaka mil 45.

Hizo mil 45 anaweza akawekeza kwenye fixed deposits kwenye mabenki au kununua hisa au dhamana za serikali, vyote hivyo vitampatia kiasi fulani cha fedha kama faida.

Hata hivyo, haya ni maelezo ya jumla jumla sana, uwekezaji unapaswa kuangalia mambo mengi zaidi ya hayo niliyoandika. Nakushauri vilevile unaweza kupata ushauri toka kwa wataalamu wa fedha na uwekezaji.

Nakutakia wewe na .mama kila la heri.
 
Tuna lengo la kutenganisha miradi tofauti,siyo kwamba yote itakwenda kwenye mradi 1
 
Kwani hapati penshion ya kila mwezi??,mfano mama yeye kila mwezi anapewa tshs 500,000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…