Mradi mkubwa wa kilimo cha kisasa cha kibiashara zao la korosho na alizeti, waanza kupitia kampuni ya Namaingo Business Agency LTD

Mradi mkubwa wa kilimo cha kisasa cha kibiashara zao la korosho na alizeti, waanza kupitia kampuni ya Namaingo Business Agency LTD

JAMHURI

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
449
Reaction score
60
Mradi mkubwaa wa kilimo cha kisasa cha kibiashara zao la korosho na alizeti, waanza kupitia kampuni ya namaingo business agency ltd.

Mkurugenzi wa kampuni ya Namaingo anapongeza uongonzi wa halmashauri ya Kibiti kwa kutekeleza mradi huo katika kitongoji cha mbawa kijiji cha Ruaruke A kata ya Ruharuke

Mkuu wa wilaya alitoa chachu kubwa na pia uongozi na kurugenzi pamoja na baraza zima la madiwani wanastahili pongezi kwani katika mikakati ya kitaifa uchumi wa viwanda kampuni imekusudia kusimamia wanachama wake kufikia azima hiyo kwa kusindika mafuta ya alizeti na pia wakati wa zao la korosho pia kuongeza thamani zao la korosho

Mkurugenzi Biubwa ameipongeza kamati ya wanachama wa Namaingo kwa kuisaidia kampuni kutimiza ndoto yake kubwa ya Tanzania mpya

Alisema kuwa mradi huu unabeba watanzania zaidi ya 4000 na utatanua kilimo katika hekari 12000 katika mfumo wa block farming

Alisema kwa anaependa kwenda kujifunza awasiliane na ofisi au kamati ili kupelekwa eneo la tukio ili atoke akiwa anafahamu hakuna kinachoshindikana chini ya jua

Mkurugenzi huyo alisisitiza kwamba watanzania tufunguke tusizoe kuona jogoo kisha ukiambiwa yupo tembo unauliza yupo km jogoo ?jogoo ni jogoo na tembo ni mnyama mwingine, alisisitiza..

IMG-20190127-WA0105.jpg
IMG-20190127-WA0102.jpg
IMG-20190127-WA0084.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama bado mnataka kuwapiga watanzania badilisheni jina mje kivingine
 
Wee jamaa unaipenda kweli familia yako? Haujui unahatarisha maisha yako?
 
Watz ni hodari kukimbilia fursa, mwishowe wanageuzwa fursa. Hawa viongozi huwa hawana mawasiliano wala kuangalia historia ya kampuni husika kuhusiana na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Ni wapi namaingo imeweza kuwavusha wananchi kiuchumi! Wakati umefika walio na madaraka ya kiserikali kuchukua hatua kwa manufaa ya wananchi wa kawaida, vinginevyo umaskini hauwezi kutoka kama akina namaingo wataendelea kupewa nafasi ya kuwalaghai wnananchi
 
Back
Top Bottom