Mradi wa nyumba 5000 wakwamishwa na Daniel Yona?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Katika pita pita yangu nimekutana na habari kuwa kampuni ya Yona iliingia mkataba na kampuni ya Enterprise Homes Tanzania Ltd ambao matokeo yake yalikuwa ni kuweza kujenzi wa nyumba zenye gharama ya chini ya dola 100,000 ndani ya miaka michache ijayo. Bahati mbaya naambiwa kuwa baada ya Benki Kuu kuja na mradi ambao nao unaweza kujenga karibu kiasi hicho hicho Bw. Yona na vijana wake wakaamua kupull out ya mkataba na kampuni hiyo ambayo Mwenyekiti wake wa Bodi ni Balozi wa zamani wa Marekani Tanzania Mch. Charles Stith.

Sasa, Wamarekani inaonekana wamekwazika.. so mkianza kusikia ubalozi wao unaanza kuwa harsh msiulize imekuwaje kwani mradi huu ulikuwa ufadhiliwe na OPIC kwa leo habari ndiyo hiyo!
 
Maumivu ya kichwa huanza taratibu...... Lakini namwaminia Muungwana, atasepa tu... wala msikonde
 
Jamani Yona,hakustahili kabisa kupewa hili jina la Yona.Halimfananii kabisa.Nitafurahi kama Ubalozi utakuwa mkali,maana mambo yetu huwa hayaendi mpaka external forces ziingilie kati.
 

Mkuu Mwanakijiji,


Kampuni ya Yona walijitoa kwa sababu gani?

Ikishakua ni ubia, kila mbia anaangalia maslahi yake...pengine hicho ndicho kilichofanyia au...kwa nini unasema wakina Yona "wameblock" huu mradi?

Kwa nini hao Wamerakani hawakutafuta mbia mwingine..?


Kwa wale ambao hawakuwahi kuusikia mradi huu, hii habari itawasaidia...

 

SSP.. kwa kweli mwenzenu nimechoka kuuliza maswali maana majibu mengine yananifanya nionekane hamnazo.
 
Bila kuwa na data wala nini nilikuwa skeptic toka day one, tuna system na individuals ambao wanafanya kitu kizuri kutokea bongo kuwa ni kimoja katika mia moja.

Wenzetu wa Ghana wana a more complex scheme with the South Koreans, $ 10 billion, nyumba 200,000, averaging at $ 50,000 per house. Nyumba 200,000 si mchezo jamani, na huu ni mpango wa serikali.Sasa huyu rais akija kuniomba kura na vitu kama ni hivi vinaonekana namwambia endelea baba, hata ukitaka kuongeza na kodi ongeza, maana tunaona zinakoenda. Hata kama kuna ufisadi hapa unaona kabisa wakulu wanauma na kupuliza. Kuna watu wame raise objection kwamba hizo hela ni nyingi sana kwa low cost houses, lakini low cost haimaanishi substandard vile vile. WaGhana probably wangeweza ku shop for a better deal au kuifanya kazi at a more affordable price, lakini give me this bad deal over a bad radar any time.

Sisi hata mtu akija kuleta msaada wa matrekta kwa wakulima tutamuomba rushwa bandarini na customs, halafu tutamuibia na matrekta yake.


South Korea in $10bn Ghana homes deal .

Ghana's cities are said to be woefully short of housing
A South Korean firm has agreed to build 200,000 homes in Ghana over the next six years at a cost of $10bn (£6.1bn), Seoul officials say.

Construction firm STX will set up a joint venture to share the cost of the project with Ghana's government.

Seoul officials say 90,000 of the homes will be owned by the Accra government - the rest will be sold.

South Korea says it intends to seek more opportunities to help build infrastructure in sub-Saharan Africa.

The country, like other rich nations, has already signed various deals in Africa giving it access to farmland to help shore up food supplies.

STX said its housing deal will involve construction in 10 cities, including the capital Accra, from 2010 to 2015.

The firm signed the deal in Seoul with Ghana's Minister of Water Resources, Works and Housing Robert Abongo.

The Korean Ministry of Land, Transport and Maritime Affairs said the deal had been completed after officials had been to Ghana to promote Korean building firms.

"Korea [has a] lack of natural resources and thus is keeping an eye on the African continent - just as developed nations and China are fiercely doing so - to secure natural resources," said a ministry statement.

"Sub-Saharan Africa is rich in natural resources but is a civil-war devastated area with poor infrastructure. Korea sees the region as a new construction market."



http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/8403774.stm
 
Binafsi ningependa kujua mpango wa BoT nyumba zake zitakuwa ni za kiasi gani? Hawa EHTL nyumba zao wanasema zitakuwa chini ya dola laki moja.. ningependa kujua BoT wanaposema "affordable" wanazungumzia prices za range gani..
 
MKJJ,

Affordable to BoT employees. Hujui affaordable to BOT Governor and Chief Justice how its differ?
 
Ni Yona yupi anazungumziwa hapa? Yona dalali au Yona mtuhumiwa wa kusigina madaraka ya ofisi ya umma?
 
Kuna mambo yanapikika underground nchi hii loh ..i wish
 
Maumivu ya kichwa huanza taratibu...... Lakini namwaminia Muungwana, atasepa tu... wala msikonde

Hiyo kwenye read huwa inaniboa sana. Hebu tu-define muungwana ni mtu wa namna gani, na unaye refer hapa ni nani?
 
Binafsi ningependa kujua mpango wa BoT nyumba zake zitakuwa ni za kiasi gani? Hawa EHTL nyumba zao wanasema zitakuwa chini ya dola laki moja.. ningependa kujua BoT wanaposema "affordable" wanazungumzia prices za range gani..


Mkuu Mkjj,

Hili la BoT tunaomba taarifa kamilifu...wengi tunajua humu kuwa BoT hairuhusiwi kufanya biashara kama za kujenga na kuuza majumba. Kazi hiyo imepewa NHC...

Sasa huu mradi wa BoT ni upi?
 
Binafsi ningependa kujua mpango wa BoT nyumba zake zitakuwa ni za kiasi gani? Hawa EHTL nyumba zao wanasema zitakuwa chini ya dola laki moja.. ningependa kujua BoT wanaposema "affordable" wanazungumzia prices za range gani..
MM, this is the basic question anyone could ask himself and BoT.
Surely, if BoT have hacked the project and reproduced the same, it is reasonable for the other company which came with the idea to drop out the idea especially if you are going to compete with a gian who a USD1million for one house is not a problem!!!!
We need affordable houses in this country, we need better houses, we need a serious real estate sector, but if BoT are going for that, it well and good and it should be very transparent and should not come as conduit of sucking the wealth of the very poor Tanzanians, i am one of those poorTanzanians!!!
 
Kama watu wanataka kuona kashfa nyingine inaitingisha nchi basi wakubali BOT kujiingiza kwenye real estate business.
BOT hawapaswi kufanya hivyo maana itakuwa ni kinyume utaratibu wa sheria za kuundwa kwa bank hiyo
 
Ndahani.. hawa watu watajiingiza kuliko luba anavyojiingiza ngozini. Yaani, hata haieleweki; watakachofanya ni kuwa hizo pesa zitapitishwa Benki Kuu ambayo itazipitisha kwenye taasisi mbalimbali za fedha na kutoa mikopo kwa kampuni binafsi za ujenzi. Ukisoma mchakato wao (I have a copy somewhere).. unaweza kupatwa na kizunguzungu..
 
Mkuu Mkjj,

Hili la BoT tunaomba taarifa kamilifu...wengi tunajua humu kuwa BoT hairuhusiwi kufanya biashara kama za kujenga na kuuza majumba. Kazi hiyo imepewa NHC...

Sasa huu mradi wa BoT ni upi?

Tembelea tovuti ya BoT Hapa halafu angalia zile press releases zao utakuta na info ya kutosha juu ya huu mradi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…