Mratibu TASAF atoa kali ya wiki, madera muwe macho na mabosi.

Mratibu TASAF atoa kali ya wiki, madera muwe macho na mabosi.

Nairobifly

Member
Joined
May 3, 2012
Posts
75
Reaction score
26
Ni mratibu wa tasaf wilaya ya Ngorongoro. Wakiwa ktk harakati za kuanza safari toka Karatu kwenda Ngorongoro dereva alimwomba bosi wake wapitie gereji kabla ya kuanza sfr ili kurekebisha matatizo madogo kwenye gari. Baada ya kufika gereji dereva alikabidhi gari na ufunguo kwa fundi, bosi wake akiwa ndani na yeye kutoka kidogo. Marekebisho ya gari hayakuwa makubwa hivyo fundi alimaliza kazi yake mapema. Bosi alikaa takiribani nusu saa akiwa anamsubiri dereva wake bila mafanikio na pia alikuwa hapatikani kwenye simu. Baada ya kuona hivyo akachukua uamuzi wa kuondoka na kumuacha dereva yule. Kilichofuata baada bosi kuondoka ni kwamba dereva ilibidi atafute usafiri private wa kwenda Ngorongoro. Taarifa zinilizopata hivi punde ni kwamba dereva yule amemburuza bosi wake polisi kwa kitendo cha kuchua gari bila ridhaa yake. Je,wandugu kati ya wawili hawa yupi mwenye makosa? Source:nimeshuhudia mwenyewe
 
Uyo bosi has to be careful dreva mwenye Kibri kama huyo kuna kitu apo sio bure.
Either bosi sio msafi au dreva ana back up ya wakubwa
Uyo dreva asingeenda uko kama bosi wake asingekuwa na mipango ya kwenda uko.
For the sake of time mgt bosi alikuwa right ingawa dreva ndo yuko responcible na gari
 
Duuuh!hii kweli kali ya wiki, kwa mimi sina jibu napita tuu, ngoja wachambuzi wa mambo waje tuone. Nitarudi later
 
Huyo bosi achunge sana.............. madereva wengi wa serikali ni usa.l..ma wa taifa.
 
Huyo bosi achunge sana.............. madereva wengi wa serikali ni usa.l..ma wa taifa.

huyu dereva ana kibur analindwa na mabos akiwa krt yeye na malaya tu licha ya kuwa na wake 3 hawamtoshi dawa yake kumpiga kijiwe au kama kuna gerej hapo afanye kaz gereji!!
 
Huyo si dereva,anawezaje kumuacha bosi alinde gari yeye aende kwa mwanamke?
 
Wote wana kosa. bosi amefanya kosa ambalo angeweza hata kutuhumiwa kwa wizi wa gari kwa sababu mwenye jukumu la kutunza na kuendesha gari ni dereva. Pia dereva amefanya kosa la kumtelekeza bosi wake. Bosi alitakiwa achukue usafiri mwingine na kuacha gari ya ofisi hapo dereva alipoiacha. Baada ya kufika ofisini angechukua hatua zinazostahili dhidi ya dereva.
 
Dereva na bosi wote ni ngunguri na hawana hekima. Boss alipaswa kuripoti polisi ili aruhusiwe kuondoka na gari, inaonesha drv ana agenda ya siri kwa boss huyu , so , boss ameingia mkenge, atakutwa na hatia kwa kuwa hana ushahidi kuwa drv alitelekeza gari. Hata hivyo, hii ni kesi ya ndani- drv alipaswa kushtaki kwa mkurugenzi wa halmashauri.
 
Kwanini bosi alibaki kwenye gari wakati linatengenezwa?
 
kwanini yeye akazima simu asibakie hapo hapo?
kama bosi wake alikuwa na haraka asingekuwa na namna zaidi ya kudrrive mwenyewe
dereva mzembe alienda wapi na kwanini awe ofline?
 
Utaratibu wa sheria za kazi hasa serikalini hauruhusu kabisa afisa/meneja/mkurugenzi au bosi yoyote kuendesha gari la serikali bila kibali. Hapo ilibidi atoe taarifa ofisini au ofisi yoyote ya serikali ili aletewe dereva aliyeajiriwa kwa kazi hiyo. (kila mtu na ofisi yake jamani)
 
dereva????? kapata wapi hii jeuri?? basi huyo bosi atakuwa bosi jina.
 
Serikali inaendeshwa kwa sheria, taratibu na kanuni, gari la serikali linakuwa chini ya dhamana ya dereva and not other wise. Uwezo wa bosi kisheria sio kujichukulia uamuzi wa kuendesha yeye bali alipaswa kumu assign dereva mwingine, au kumtaarifu DAP kuwa kuna dharura dereva ame obscond porini, hivyo bosi akafanya initiative kuokoa jahazi.

Kimakosa ya kiutendaji, mwenye kosa ni bosi maana 30 min is not tuu much to wait!. above that ndio too much!.

Kwa sheria za kazi, yule dereva atatakiwa kundika maelezo na ataishia kupewa onyo kwa uzembe kazini na kuhamishwa kituo cha kazi. Bosi ataandika tuu maelezo na issue itaishia hapo.

Tukija kwenye haki, mabosi wana haki zaidi!.
 
Back
Top Bottom