Habari Wakuu?
Nilikuja hapa jukwaani 29.04.2014 na kuomba msaada wa wazo la biashara.
Nashukuru wote mlio changia, kwani May Katikati nilianza kununua pens na daftari & stationaries zingine na kuuza chuoni.
Hivi ninazungumza nina mtaji wa sh. milion moja na laki sita na nazidi kutafuta fursa za kuwekeza kusonga mbele.
Ahsante sana Bulldog, King Octavian, Mama Joe, delly, Mbunda E, Coping Strategy, maringeni Na Exorcist na wengine wote mlio changia chochote pale, Mungu awabariki.
Msinichoke nikija kuomba msaada wa mawazo zaidi.
VIVA JF!!
Umefanya vizuri kurudi jukwaani kushukuru, hawa sasa ni ndugu zako,wala hawatakuchoka, na pengine leo wamefurahi kuona michango yao imejibu. Nitakupa ushuhuda wangu.
Mzee mmoja alinisaidia,niliona aibu kurudi kushukuru sababu nilikuwa apeche alolo,ila aliniusia kuwatendea wengine vizuri. Miaka imekatika mingi,mwaka juzi nilifanya kazi ya uwekezaji ya dada mmoja vizuri. Mwaka jana mwishoni ndio nimekuja kugundua, yule dada ni mjomba wake na yule mzee aliyenisaidia. Mzee aliniinua mimi na mimi nimekuja kumlipa yeye bila kujua kama narudisha fadhila zake. Hata kama huna kitu na ukawa na dhamira safi Mungu anaona, wewe shukuru tu.