Mrejesho: Manunuzi ya mtandaoni (ebay)

Posta yetu wakijiboresha na kuwa waaminifu(maana kuna watu hawaiamini posta kwa vitu vya thamani).....watatengeneza fedha sana kwenye online logistics.
 
Posta yetu wakijiboresha na kuwa waaminifu(maana kuna watu hawaiamini posta kwa vitu vya thamani).....watatengeneza fedha sana kwenye online logistics.
Yah register na EMS wako makini.. Vinavyopotea ni vile vinavyotumwa kwa P. O. BOX
 
Mmh namba tena usije ukawa ni member wa mjengoni..
Mjengoni gani tena.....hapana mi mbona nmekupa namba yangu boss nkaona kama w itakuwa shida kunipa yako nkakuomba ww ndo ujicheki unajua hz text naona zinakuwa ngumu kueleza kila jambo ndo maana naona nirahis kumpata mtu na kuongea nae moja kwa moja unapata kujua kwa undani
 
Safi sana
 
Haya nmekupata... Nilizan ww ni mzee wa magogoni.. Ntakutafuta nikupe details zote
 
Mimi huwa nanunua mara nyingi sana online kutoka Amazon. Issue ya kuibiwa ilikuwa unanipa wasi wasi sana.
Ninachofanya ni kuwa makini tu na emails za pale nitakaponunulia iwe Amazon, ebay ama Alibaba.
Pia kwa sababu ya uoga, nilifungua account special ninayotumia manunuzi ya online. Nikitaka kununua kitu basi huweka kiasi kinachotakiwa pekee huko. Kawaida huwa situnzii pesa zangu huko (najua ni uoga wangu huo lakini I hope huwa unanisaidia hata kama wadukuaji wakichungulia wanakuta zero).
 
Nimetumia 2 year biashara ya mtandao, sasa nina 2 weeks tangu nimetua najipanga kuendeleza shopping katika site kama Amazon, Ebay, 6.pm, Walmart, Alibaba na site nyingine nyingi. Experience ya nje mzigo unaletewa mpanga mlangoni kwako sababu nyumba zote ziko mapped so ku-locate mzigo inakuwa very easy. Tatizo nililosikia zamani kwa nchi za Africa ni kuwa mizigo mara nyingi inafika posta sababu ya changamoto ya zip code, area code, n.k. So wengi walilallamika kuwa mizigo yao iliishia kupotea kwenye ofisi ya posta. Ukipata statement ya delivering kwenye posta ya nchi yako. Jamaa wa posta wantembea nayo alafu wanakujibu bado haujafika/hawajapata..........................so let me try and see the truth
 
Usisahau kutuletea mrejesho mkuu..
 
Cha msingi usifungue link ambayo huielewi elewi.. Wala kujibu msg ambayo unawasi was nao...
 
Hukufuata njia sahihi wakati wa manunuzi...
Mimi ni mzoefu na nimefanya manunuzi sana ebay, amazon na alibaba. Nilichogundua ni kwamba mitandao ya ebay & amazon haiwalengi watu waishio Afrika, labda alibaba yenye bidhaa nyingi za kichina.
 
Mimi ni mzoefu na nimefanya manunuzi sana ebay, amazon na alibaba. Nilichogundua ni kwamba mitandao ya ebay & amazon haiwalengi watu waishio Afrika, labda alibaba yenye bidhaa nyingi za kichina.
Bado sijakupata... Inamana bidhaa zao hazifiki afrika?
 

Zinafika ila uhakika sio mzuri kama kwa ulaya na marekani. Ebay na Amazon ni kama kupatana tu, hawatoi huduma za shipping Afrika, so your own risk.
Kuna wanaotoa free international shipping na ambao hawatoi.. Ni jukumu lako kuangalia yupi anatoa wakati wa uchaguzi wa bidhaa.. Wengine wanatoa ila yapaswa kulipia shipping.. Mi nafikiri mdau unapaswa kujifunza zaidi haya maswala kabla ya kulinganisha ebay na kupatana
 
Binafsi nina shop sana na EBay....
Na nipo mkoani huku ila vitu vinafika poa kabisa ila address yangu niliweka P.O.Box ;
Kwa ushauri wako nitarekebisha nianze kutumia Code +255.

Ila kuna changamoto nimepata Amazon nimenunua kitabu ila hakifiki,
Nikawasiliana na watu wao wa Customer Service ila wakasema wanatuma tena ila mpaka sasa hola na ETA ilikuwa Feb 15.....
Sijui nini ilikuwa mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…