Mrejesho: Ndoto inayojirudia kwa Miaka 12 sasa!

Mrejesho: Ndoto inayojirudia kwa Miaka 12 sasa!

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,301
Reaction score
8,706
Hii Ndoto inanisumbua Mwaka wa 12 Huu.

Baada ya kutafuta nasaha kwa ndugu jamaa na marafiki, nilifanikiwa leo kupata nasaha kwa rafiki yangu mmoja...akanipeleka mahali kwa Mmama mmoja hivi (I Guess ni Mpiga Ramli), basi akaniambia nimtajie jina langu nami nikamtajia.....katika kufanya mambo yake akaniambia kuna Jirani yenu ambaye mna kaundugu fulani alishawahi kuchukua Daftari,unywele na ukucha wangu.....anasema hivo vitu vimewekwa kando ya mto ndio maana hio ndoto haiishi kujirudia.

Anasema kupitia hivo vitu vilivyochukuliwa....kuna weakness nyingi zinajitokeza na wengine ambao wana nia mbaya na mimi basi hunidhuru kirahisi.

Aliniambia vitu vingine tofauti na ndoto ambavyo vina ukweli 100%.....sasa akaniambia inatakiwa nimtafutie mtu atakaeweza kwenda kunichukulia hivo vitu....kama jina lake litafit....na kwa kweli mimi sijui jina la mtu yeyote anayechukua vitu vya mtu vilivyochukuliwa kichawi..!

Basi naombeni wanandugu kama kuna mtu anamjua mtu mwenye uwezo wa kurudisha vitu vya mtu vilivyochukuliwa kichawi anisaidie tu......Popote Tanzania naweza kuenda kikubwa nisaidie Jina na Anapokaa!

Maji yamefika Shingoni.!
 
Kwann huyo mpiga ramli asikutibu tuu,unafikiri utampata nani wa kwenda kukuchukulia hivyo vitu vyako ambavyo vilichukuliwa kichawi sidhan
 
Kwann huyo mpiga ramli asikutibu tuu,unafikiri utampata nani wa kwenda kukuchukulia hivyo vitu vyako ambavyo vilichukuliwa kichawi sidhan
Mkuu watu wanatest Majina yao yakikataa wanakuambia ucheki yako
 
Nenda kigoma sehemu inaitwa kagera nkanda au kagaze kibondo
 
Tafuta SHEHE akuangushie ALAL BADIRI ya NGUVU... umshitakie MUNGU... kama kuna mtu yeyote amekufanyia mabaya basi yamrudie mwenyewe kwa NIA YAKE ,,, aliyokukusudua huyo MCHAWI,,, basi yampate yeye,, hyo ndy DAWA,,, HUNA NAMNA,,,
 
Tafuta SHEHE akuangushie ALAL BADIRI ya NGUVU... umshitakie MUNGU... kama kuna mtu yeyote amekufanyia mabaya basi yamrudie mwenyewe kwa NIA YAKE ,,, aliyokukusudua huyo MCHAWI,,, basi yampate yeye,, hyo ndy DAWA,,, HUNA NAMNA,,,
asantee
 
In God I trust, out of his voice he created both of us! My advice don't find anyone to send, just tell God and he will deal with it no matter if it exist or not!
 
hizo trouble zote za nini....piga goti sali mlilie Mungu wako...yeye ni mkubwa kuliko huyo mpiga ramli wako...ni mkubwa kuliko huyo unaemtafta akakuchukulie hayo madudu yako...ni YEYE TU ATOSHA....na ni yeye tu ndo ataekusaidia...
 
In God I trust, out of his voice he created both of us! My advice don't find anyone to send, just tell God and he will deal with it no matter if it exist or not!
Nahisi imani yangu huko haitotosha
 
kaka mshana jr you are needed here plz
Mtafute mshana
Naomba sana nishauri asiende popote patakapohusika na nguvu za giza.. Huko haendi kutengeneza bali kuharibu zaidi kwa ufumbuzi wa muda mfupi
Kama ni kweli hivyo vitu vilichukuliwa haviwezi kuwepo mpaka leo hii.. Ni haiwezekani kabisa
Mimi tiba yangu kwake ni ileile kuogea chumvi ya mabonge na kujipaka kitunguu saumu kwenye paji la uso na viganjani.. Ajaribu hiyo kwa wiki mbili kwanza... Afanye hivyo akienda kulala
Sasa hivi sio muda tena wa kutafuta kilichochukuliwa kwakuwa kilishatumika kama malighafi ya kudhuru... Sasa hivi ni kutafuta kuliondosha peporoho lililotengenezwa na hivyo vitu
Zaidi angefunguka kwa uwazi hayo mengine ingesaidia pia
 
Naomba sana nishauri asiende popote patakapohusika na nguvu za giza.. Huko haendi kutengeneza bali kuharibu zaidi kwa ufumbuzi wa muda mfupi
Kama ni kweli hivyo vitu vilichukuliwa haviwezi kuwepo mpaka leo hii.. Ni haiwezekani kabisa
Mimi tiba yangu kwake ni ileile kuogea chumvi ya mabonge na kujipaka kitunguu saumu kwenye paji la uso na viganjani.. Ajaribu hiyo kwa wiki mbili kwanza... Afanye hivyo akienda kulala
Sasa hivi sio muda tena wa kutafuta kilichochukuliwa kwakuwa kilishatumika kama malighafi ya kudhuru... Sasa hivi ni kutafuta kuliondosha peporoho lililotengenezwa na hivyo vitu
Zaidi angefunguka kwa uwazi hayo mengine ingesaidia pia
Mkuu Mshana Mganga huyo kaniambia hio hali ya vitu vyangu kuchukuliwa....inatengeneza weakness flani hadi nadhurika kirahisi so itabidi vifuatwe
 
Mkuu Mshana Mganga huyo kaniambia hio hali ya vitu vyangu kuchukuliwa....inatengeneza weakness flani hadi nadhurika kirahisi so itabidi vifuatwe
Sio kweli kabisa... Ungekuwa unadhurika kirahisi usingekuwa hai mpaka sasa! Kinachokutesa ni hofu uliyoamua kuipa nafasi katika mustakabali wako! Vita vya kiroho si mchezo ungekuwa dhaifu huna kinga ya kiroho zamani sana ungeshaondoshwa
Anyway huo ni mtazamo wangu tu na nilichokushauri utumie ni tiba yenye nguvu sana
 
Back
Top Bottom