Mrejesho: Safari yangu Gabon mwaka jana

Shinbet18

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2018
Posts
255
Reaction score
263
Good morning my beloved members! Natumai mmeamka salama.Leo niwape nilicho kiona mwaka jana huko Gabon.

Nilifikia kwenye jiji la Port- gentil Kwa matembezi ya kawaida kuangalia fursa za biashara.Jiji lile pia wanaliita Mandji.Nilipo pokelewa na mwenyeji wangu katika uwanja wa ndege wa port gentile nilifikia kwake kama yeye alivyofikia kwangu alipokuja Tanzania.

Asubuhi yake akanipeleka mitaa tofauti ya lile jiji kuangalia biashara zinavyoendeshwa.Jiji lilikuwa safi na lenye mpangilio unaovutia sana mpaka raha.

Kilichonistajabisha ni unifomu za biashara.Yaani kila duka au bao ni biashara aina moja tu.Sijaona mtu aliye changanya nguo sukari dawa mafagio pamoja.

Kama ni nguo basi hutaona kingine.Kama ni matunda hutaona kingine zaidi ya matunda.Kama ni electronics hutaona mchele hapo kama wabongo wanavyo changanya bidhaa.

Mwenyeji wangu Oliver akaniambia huo ni utaratibu waliojiwekea wafanyabiasha kote Gabon.Nilivutiwa sana.

Nashauri bongo pia tufanye hivyo kuepusha kupokonyana wateja asanteni.
 

Anza kufanya wewe kwanza sio unashauri wenzio tu .. anza sasa kisha uje utupe mrejesho
 
Upuuzi! bidhaa zilivyo nyingi utakuwa na maduka mangapi? Hujakatazwa kuanzisha ya aina hiyo hapa bongo..ila haya yetu yaliyohanganywa pia ni style yake mi ningekuwa Gabon ningechanganya
 
Jirani yetu baada ya kumaliza form IV miaka hiyoooo ya 90 alikwenda kubangaiza Guinea. Sijui alianza vipi lakini kujua kwake English kulimsaidia sana kwani ile nchi wanaonge ki-Portuguese.

Alikuwa handsome na mtoto wa mjini, ninasikia katika kujichanganya akakutana na mtoto wa rais wakawa ma best.
Alipata michongo ya serikalini na tender. Pesa ilimkubali. Vijana walimuua bwana, Hakuna aliye jua kiini cha kifo chake, mali yake yote ilipotea

So sad.
 
Story yako inatufunza nn
 
Gabon ndio ulifuata ivyo tu, mbona ata mtaa wa agrey wanauza simu tu.
 
Mimi baada kusikia mrejesho kutoka Gabon nikatarajia fursa zinazopatikana huko na sisi wafanyabiashara wahapa tubangaize na sisi tuende kumbe unatuambia uniformity of products sasa si kawaida tu. Ila mkuu mimi nakuomba kwa niaba utupe fursa za huko Gabon na sio hizi story.
 
Ndio maana hapa bongo wafanya biashara wengi wanagombana kila siku TRA. kwa sababu duka moja unakuta mtu anauza nguo mara anauza mchele hapo anauza na radio bado ana m pesa.
Inamaana hapo TRA wakija wanakupigia hesababu ya maduka matatu.
 
Fursa iko wapi hapa? Hizi akili Trump akiwaambia shit hole, mnaanza kutoka povu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…