Mrejesho wa FIESTA DSM 2017

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Usiku wa kuamkia leo pale leaders kulikuwa na kilele cha Fiesta huku waandaaji wakijipambanua na kauli mbiu ya 100% local, yaani wasanii wote watumbuizaji wanatoka nyumbani.

Watazamaji-
Watazamaji kiukweli walijitokeza wengi hasa ukizingatia kiingilio kilikuwa sh
10000 na promo iliyofanyika watu hawakusita kwenda

Watumbuizaji/ wasanii-

Wasanii walijitaidi kuvaa vizuri kwa namna ambayo waliona watandeza.

Jukwaani-

Waandaaji walijitaidi kuwawezesha wasanii waimbe live band na hapa ndo tatizo kubwa lilipotokea
Wasanii wengi hawajui kuimba live band huku wakijiconnect na mashabiki hili lilisababisha show kupooza hakukuwa na shangwe

Wasanii wakifika jukwaani wanapiga story nyingi mpaka wanaboa mfano wasanii Jux na Vanessa mdee walitumia muda mwingi kuombana msamaa kuhusu mapenzi yao kuliko kupiga show

Kuchanganya Bongo movies na kuimba jukwaani

Mfano kitendo cha kuwapandisha jukwaani Ebitoke, Mama Ashura na Tausi kulibadilisha maana kutoka tamasha la music hadi kuwa la maigizo zikawa drama nyingi jukwaani hadi zinaboa

Ommy dimpoz kiukweli alizingua sana sijui tatizo hajui kuimba na live banda au alikamia sana kiwango chake kilikuwa chini sana kuliko hata wasanii wachanga

Wasanii waliofanya Vizuri

Rostam- roma na stamini walijitaidi sana kuleta amsha amsha

Rich Mavoko- alijikita zaida kuimba kuimba kuliko kupiga story jukwaani inawezekana kwasababu sio muongeaji sana.

Ben paul- alijitaidi kuwa mbunifu na kuimba vizuri alianza kuaribu alipompandisha ebitoke na kuleta maigizo

Nyandu toz na mr blue- walipiga show ya maana kuliko hata wale waliokuwa midomoni kwa watu

Jux na vanesa - walijitaidi japo walikuwa wanaboa kwa maongezi mengi jukwaani

Alikiba- alikiamua japo kulikuwa na tatizo la sauti, sijui ni mic yake ilikuwa mbovu au vyombo vya bendi ndo vilikuwa vinazingua, nadhani ndo kilichosababisha asiwe kwenye ubora wake.

Hitimisho

100% local ni wazo zuri la kujenga kujiamini kwa wasanii wetu ila nadhani bado tunapaswa kujifunza kutoka kwa wasanii kama Wizkid, Davido na Patoranking hawa wakiwa wanaimba live.
 
Kiba 100 mpuuzi alizingua, ROSTAM kama kawa, Ben Pol saafi.
 
wewe ulikuwepo jana na hadi sasa upo macho....!!!!?
au umesimuliwa hayo
 
Mimi nilifurahia ile njia ya kuingilia kwenye uwanja wa fiesta. Njia ilikuwa ni pana sana kama ile njia iendayo Jehanam!😱 Yani kwa ukubwa ule wa njia, hata semi trailer ingeweza kugeuzia pale. Mapolisi jana walikuwa ni wapole kama malaika. Hii inaonekana jeshi limetoa kozi nzuri ya customer care. Misosi ilikuwa iko bomba n.k... Japo niliwahi kuchomoka ila the atmosphere was nince!
 
Ndo naamka muda huu. Show ilikuwa kali sana.

Kalapina alifunika mno.
 
Mi kiukweli niliikubali sana show ya Daz Nundaz,daaah jamaa wanatisha.

Bahati mbaya Gangwe Mob walizingua but all in all burudan ilikuwa fresh.
 
Kila nikifungua uzi JF nadhani Kitila naye ame comment.
 
Kama wewe ni Mu ISLAM uliekamilika, Jana umekwenda huko... Jiandae na majibu sahihi Siku yako yamwisho. Maisha yetu nimafupi sana hapa duniani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…