makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Dodoma. Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Augustine Mrema amedai baadhi ya wajumbe wanataka kuligeuza bunge hilo ‘shamba la bibi' kwa kudai posho zaidi kwa kisingizio cha kupanda gharama za maisha.
Akizungumza mjini hapa jana, Mrema alisema wajumbe wanaoshawishi wenzao kudai posho zaidi ni wale waliopelekwa kuishi kwenye hoteli za bei ya juu kati ya Sh100,000 na Sh220,000 kwa siku.
Mrema alisema Sh300,000 wanacholipwa kinatosha kwa sababu kuna hoteli nzuri za kati ya Sh15,000 hadi Sh40,000, ambazo zina hadhi na sifa ya kuishi wajumbe wa Bunge la Katiba.
"Mjumbe ameamua kwenda kuishi chumba cha Sh200,000 wakati akijua atalipwa Sh300,000 halafu analalamika kupanda kwa gharama za maisha… hizi gharama zimetengenezwa,"alisema Mrema.
Alitaka kamati ya watu sita iliyoundwa na Bunge kufuatilia suala la posho, ifanye uchunguzi nyumba za kulala wageni walizofikia wajumbe kubaini ukweli wa kupanda kwa gharama.
Mrema alisema nyumba nyingi za kulala wageni ikiwamo yake haikuorodheshwa kwenye hoteli walizopewa wajumbe.
"Mimi hapa kwangu vyumba vinaanzia Sh20,000, bado tunaweza kuzungumza lakini haikuingizwa kwenye orodha… nakwambia huu ni mchongo ili wajumbe waende nyumba fulani-fulani," alisema Mrema na kuongeza:
"Ughali wa maisha unatengenezwa, zipo tupu na watu wamekimbilia hizo za ghali ili waje wadai posho zaidi… Hayo ni matakwa kama wanataka waje huku kwangu maisha ni bwerere wasitake kuingiza Serikali gharama."
Alihoji sababu za wajumbe hao pekee kupiga kelele za kuongeza posho, ilhali kuna makundi mengine yanayofanya kazi hizohizo.
Source: Mwananchi newspaper
My take: Mzee wa Kiraracha umenena vema. Kumbe bado unaonekana kuwa na busara na hikma na umenikumbusha zile enzi zako ulipokuwa N/Waziri Mkuu ukitoa amri za siku 7 kwa majambazi na vibaka kusalimisha silaha zao. Hongera sana akwi. Tunataka Wabunge wengine wa Bunge la Katiba hasa wale wa CCM waige mfano wako na wawe na mtazamo kama wa kwako ili hatimaye muweze kutimiza adhima na malengo yaliyowapeleka Dodoma ambayo ni ya kuwatengenezea Watanzania Katiba mpya.
Akizungumza mjini hapa jana, Mrema alisema wajumbe wanaoshawishi wenzao kudai posho zaidi ni wale waliopelekwa kuishi kwenye hoteli za bei ya juu kati ya Sh100,000 na Sh220,000 kwa siku.
Mrema alisema Sh300,000 wanacholipwa kinatosha kwa sababu kuna hoteli nzuri za kati ya Sh15,000 hadi Sh40,000, ambazo zina hadhi na sifa ya kuishi wajumbe wa Bunge la Katiba.
"Mjumbe ameamua kwenda kuishi chumba cha Sh200,000 wakati akijua atalipwa Sh300,000 halafu analalamika kupanda kwa gharama za maisha… hizi gharama zimetengenezwa,"alisema Mrema.
Alitaka kamati ya watu sita iliyoundwa na Bunge kufuatilia suala la posho, ifanye uchunguzi nyumba za kulala wageni walizofikia wajumbe kubaini ukweli wa kupanda kwa gharama.
Mrema alisema nyumba nyingi za kulala wageni ikiwamo yake haikuorodheshwa kwenye hoteli walizopewa wajumbe.
"Mimi hapa kwangu vyumba vinaanzia Sh20,000, bado tunaweza kuzungumza lakini haikuingizwa kwenye orodha… nakwambia huu ni mchongo ili wajumbe waende nyumba fulani-fulani," alisema Mrema na kuongeza:
"Ughali wa maisha unatengenezwa, zipo tupu na watu wamekimbilia hizo za ghali ili waje wadai posho zaidi… Hayo ni matakwa kama wanataka waje huku kwangu maisha ni bwerere wasitake kuingiza Serikali gharama."
Alihoji sababu za wajumbe hao pekee kupiga kelele za kuongeza posho, ilhali kuna makundi mengine yanayofanya kazi hizohizo.
Source: Mwananchi newspaper
My take: Mzee wa Kiraracha umenena vema. Kumbe bado unaonekana kuwa na busara na hikma na umenikumbusha zile enzi zako ulipokuwa N/Waziri Mkuu ukitoa amri za siku 7 kwa majambazi na vibaka kusalimisha silaha zao. Hongera sana akwi. Tunataka Wabunge wengine wa Bunge la Katiba hasa wale wa CCM waige mfano wako na wawe na mtazamo kama wa kwako ili hatimaye muweze kutimiza adhima na malengo yaliyowapeleka Dodoma ambayo ni ya kuwatengenezea Watanzania Katiba mpya.