Mrema: Kura ya siri ni unafiki

Mrema: Kura ya siri ni unafiki

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,277
Reaction score
8,860
Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustino Mrema amesema watu wanaotaka kura ya siri bungeni ni wanafiki huku Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira akiahidi kuonyesha wazi msimamo wake na kwamba ukiathiri ustawi wa taifa anataka aadhibiwe angali hai au mfu.

Wakizungumza kwenye mahojiano na televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jana, Mrema na Wassira walisema wao wanataka kuonyesha msimamo wao.

Mrema alisema wajumbe wanaotaka kura ya wazi kwa kisingizio cha kuhofia kushughulikiwa na vyama vyao ni wanafiki na kuwataka waige mfano wake.

Naye Wasira alisema hakuna sababu inayoweza kuhalalisha kura ya siri katika kuamua mambo nyeti ya kitaifa kama kuunda na kupitisha Katiba Mpya.

Alisema kama ni suala la msimamo wa mtu kutofautiana na ule wa chama au kundi lililomweka kwenye nafasi hiyo, utafahamika kupitia kwenye mijadala yake, ndani ya Bunge, Kamati au katika mazungumzo yake ya kawaida.

“Mimi msimamo wangu ni serikali mbili kwa sababu ni wenye historia inayoeleweka kuwa una dhamira ya kuunda mfumo wa muungano endelevu na nyingine nyingi zilizo njema kwa watu wote, nitasimamia msimamo huo na ikitokea ukaleta madhara kwa taifa, hata nikishakufa watoto na wajukuu wangu waje tu kwenye kaburi langu, wanichape viboko,” alieleza Wassira.

Mrema alisema alikuwa waziri akaweka wazi msimamo wake uliokuwa kinyume na chama chake wakati huo (CCM).

“Kila mtu anafahamu yaliyonikuta, hadi leo yapata miaka 20 sijalipwa mafao yangu. Wananchi wangu si wamenirudisha bungeni? Anayeficha msimamo wake ni mnafiki, wala hafai kuwa kiongozi,” alieleza Mrema, ambaye alitimuliwa uwaziri mwaka 1994.
 
Ni kweli mkuu kwanini ufiche msimamo wa mstakabali wa nchi yako.hawa jamaa wanataka kuficha ni hatari kwani tabia hiyo wanayo wasaliti
 
Ni kama ambavyo ungemhoji mh.jar people unategemea jibu gani?Ni lazima uwe ni mtu unayejitegemea ktk kufikiri
 
Hamjasikia kuwa kuna chama kimoja kimewaeleza wajumbe wanachama wake kuwa atakayepingana na msimamo wa chama ni mhaini na chama kitamshughulikia? Mbona rais wa nchi anachaguliwa kwa kura ya siri na cku zote hawakusema ni unafiki, nadhani wanaopingana na utamaduni wa kawaida wa kupiga kura ndio wanafiki, maana wana lengo lao binafsi wanalotaka kulifikia kupitia kura ya wazi.
 
Na hapa Mrema ajue kura si sawa2 na misimamo ya kisiasa. Mfano wake uko tofauti na anachokiongelea
 
Mrema ni mtu wa CCM je tutegemee tofauti na alivyosema? yeye aendelee kuwatumikia mpaka hapo mungu atakapomkumbuka na ndio hapo tutabaki na historia ya kiumbe fulani ambaye aliitwa Mrema
 
Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Augustino Mrema amesema watu wanaotaka kura ya siri bungeni ni wanafiki huku Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira akiahidi kuonyesha wazi msimamo wake na kwamba ukiathiri ustawi wa taifa anataka aadhibiwe angali hai au mfu.

Wakizungumza kwenye mahojiano na televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jana, Mrema na Wassira walisema wao wanataka kuonyesha msimamo wao.

Mrema alisema wajumbe wanaotaka kura ya wazi kwa kisingizio cha kuhofia kushughulikiwa na vyama vyao ni wanafiki na kuwataka waige mfano wake.

Naye Wasira alisema hakuna sababu inayoweza kuhalalisha kura ya siri katika kuamua mambo nyeti ya kitaifa kama kuunda na kupitisha Katiba Mpya.

Alisema kama ni suala la msimamo wa mtu kutofautiana na ule wa chama au kundi lililomweka kwenye nafasi hiyo, utafahamika kupitia kwenye mijadala yake, ndani ya Bunge, Kamati au katika mazungumzo yake ya kawaida.

“Mimi msimamo wangu ni serikali mbili kwa sababu ni wenye historia inayoeleweka kuwa una dhamira ya kuunda mfumo wa muungano endelevu na nyingine nyingi zilizo njema kwa watu wote, nitasimamia msimamo huo na ikitokea ukaleta madhara kwa taifa, hata nikishakufa watoto na wajukuu wangu waje tu kwenye kaburi langu, wanichape viboko,” alieleza Wassira.

Mrema alisema alikuwa waziri akaweka wazi msimamo wake uliokuwa kinyume na chama chake wakati huo (CCM).

“Kila mtu anafahamu yaliyonikuta, hadi leo yapata miaka 20 sijalipwa mafao yangu. Wananchi wangu si wamenirudisha bungeni? Anayeficha msimamo wake ni mnafiki, wala hafai kuwa kiongozi,” alieleza Mrema, ambaye alitimuliwa uwaziri mwaka 1994.

Niliwaona jana, ila nilijaribu kuwaangalia kwa makini, nikagundua ni kwa kuwa Msimamo ulishawekwa, haikuwa dhati ya kutoka moyoni!
 
Mrema ndo mwana mageuzi wa kweli. Wengine wanaiga tu
 
#Kibo habari yako imejichanganya....Mwanzo umesema Mrema anapinga kura ya siri....Then, kuna mahali unasema huyo Mrema hataki kura ya wazi....sasa anaunga mkono kura ipi?
 
Ni kweli mkuu kwanini ufiche msimamo wa mstakabali wa nchi yako.hawa jamaa wanataka kuficha ni hatari kwani tabia hiyo wanayo wasaliti

SaidSabke, Kwa mtazamo huo waweke kipengele kwenye katiba kuelekeza mambo yote yenye kugusa mstakabali wa nchi yaamuliwe kwa kura za wazi ( mf. uchaguzi wa Rais na wabunge) ili wananchi waone wazi kinachoendelea.
 
Mi nataka kura ya wazi kura ya maoni kupitisha katiba mpya.

Ringo Edmund, isiishie kwenye maoni tu , bali iwe ndo mwongozo wa kikatiba kwa chaguzi zote zitakazofuata baada ya katiba mpya kuanza kutumika
 
kufichaficha noma tunatakq kitu live

uchaguzi wa rais siyo jambo la kitaifa?mbona kura inakuwa ya siri?nchi yeyote inayoongozwa kwa mfumo wa demokrasia kura ya siri ndio inakubalika ili kutoa uhuru kwa mpiga kuru kufanya aamuzi sahihi ya nafsi.
kwa maana hiyo kura wazi hiyo haikubaliki hata kidogo kwani itamnyima mjumbe uhuru.
 
Back
Top Bottom