Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mrisho Gambo, ametembelea mradi wa ujenzi wa Barabara ya Engosheraton jijini Arusha na kumtaka mkandarasi wa mradi huo, Jiangxi GEO, kuongeza kasi ya utekelezaji.
Akizungumza baada ya ziara hiyo, Gambo amesema barabara hiyo ilitakiwa kuwa imefikia asilimia 86 ya utekelezaji, lakini hadi sasa imefikia asilimia 60 pekee, kwa mujibu wa wasimamizi wa mradi.
Mkandarasi huyo amekiri kuchelewa kupeleka mitambo kwa karibu wiki tatu na ameahidi kuanza kupeleka mitambo yote inayohitajika kuanzia kesho.
Aidha, amesisitiza kuwa miradi ya miundombinu inapaswa kusimamiwa kwa ufanisi ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.
Akizungumza baada ya ziara hiyo, Gambo amesema barabara hiyo ilitakiwa kuwa imefikia asilimia 86 ya utekelezaji, lakini hadi sasa imefikia asilimia 60 pekee, kwa mujibu wa wasimamizi wa mradi.
Mkandarasi huyo amekiri kuchelewa kupeleka mitambo kwa karibu wiki tatu na ameahidi kuanza kupeleka mitambo yote inayohitajika kuanzia kesho.
Aidha, amesisitiza kuwa miradi ya miundombinu inapaswa kusimamiwa kwa ufanisi ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.