Mrisho Gambo: Bajeti Haijatoa Ahueni yoyote Sekta ya Utalii, Wanaenda Kuiua

Mrisho Gambo: Bajeti Haijatoa Ahueni yoyote Sekta ya Utalii, Wanaenda Kuiua

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mrisho Gambo akichangia Bungeni kwenye Bajeti iliyopendekezwa, ameielezea kutotoa ahueni yoyote kwenye sekta ya utalii iliyoyumba kutokana changamoto za ugonjwa wa Covid.

Amesema mchango wa utalii umeshuka kutoka asilimia 17.5 mpaka asilimia 10.7 na mapato yamepungua kutoka bilioni 584 mpaka bilioni 89 kulingana na taarifa ya wizara.

Amesema changamoto kubwa zimejitokeza hasa kwenye ajira akitolea mfano Arusha mahoteli mengi yameathirika, tour operators, waongoza watalii, madereva, wapagazi, wapiga mahema na staff wa maofisini wako hoi.

Gambo amesema pamoja na matatizo yote hayo, wizara ya maliasili na utalii na serikali imekuja na suluhisho la kuongeza tozo.

Gambo amesisitaza wizara ya maliasili na Utalii wasipoangaliwa wanaenda kuiua sekta na ameiita ni corona na mbili nchini.

Ameshauri Tozo husika zisitishwe.

 
Huyu ndiye yule Mrisho Gambo au wako Double
huhkoby.png
 
Mrisho Gambo akichangia Bungeni kwenye Bajeti iliyopendekezwa, ameielezea kutotoa ahueni yoyote kwenye sekta ya utalii iliyoyumba kutokana changamoto za ugonjwa wa Covid.

Amesema mchango wa utalii umeshuka kutoka asilimia 17.5 mpaka asilimia 10.7 na mapato yamepungua kutoka bilioni 584 mpaka bilioni 89 kulingana na taarifa ya wizara.
Ukiambiwa hawa watu walikuwepo kipindi Cha utawala wa mwenda kuzimu unaweza kukataa kabisa🙄🙄🙄
 
Kwa hoja hizo Mh. Gambo ameongea vyema kabisa na kuonyesha ana uelewa mpana wa sekta ya utalii na athari hasi za tozo mpya katika kipindi hiki cha janga na athari za gonjwa la UVIKO.
 
Anaongea madini, japo ni mnafiki. Ila tusiyapuuze madini yake. Bajeti hii kwenye utalii imejaa madudu tu, yule jamaa mcheza gofu amepwaya sana. Mkenda ile wizara ingemfaa zaidi.
 
Back
Top Bottom