Tetesi: Mrisho Gambo kuhamia ACT Wazalendo?

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Kuna habari za chini chini kwamba Mrisho Gambo yuko katika maongezi ya ngazi ya juu ili kuona uwezekano wa kuhamia ACT Wazalendo.

Tetesi hizo zinatokana na upepo mbaya kisiasa jimboni ambao unachochewa na mahusiano mabaya aliyonayo na viongozi wote wa mkoa mzima wa Arusha katika chama na serikali. Gambo amekuwa akituhumiwa kuwachongea maneno ya uongo viongozi wenzake Mkoa wa Arusha na kuendesha siasa za fitna na majungu
 
Hakuna mwanaccm anaweza kufanya siasa nje ya ccm, kwani wanaccm wote hutegemea mbeleko ya vyombo vya dola na sio ushawishi wa hoja.
 
Hakuna mwanaccm anaweza kufanya siasa nje ya ccm, kwani wanaccm wote hutegemea mbeleko ya vyombo vya dola na sio ushawishi wa hoja.
Waanzilishi wa chadema wote ni wana CCM, chadema ni extension ya CCM, plan B ya Lumumba
 
Waanzilishi wa chadema wote ni wana CCM, chadema ni extension ya CCM, plan B ya Lumumba
Waanzilishi wengi kwa mazingira halisi wangetoka ccm wakati huo, kwani nchi ilikuwa ya chama kimoja. Hivyo wakati ule ndio ilikuwa uhalisia. Lakini haina mahusiano na ulichoquote toka kwangu.
 

Hawezi kuwa mjinga hivyo, maana atapotea kwenye siasa kama Nyalandu
 
Waanzilishi wengi kwa mazingira halisi wangetoka ccm wakati huo, kwani nchi ilikuwa ya chama kimoja. Hivyo wakati ule ndio ilikuwa uhalisia. Lakini haina mahusiano na ulichoquote toka kwangu.
Message sendi
 
Makonda kamtia la kati Mrisho Gambo.
Jimbo linagawanywa mara mbili. Tume ishasema ni moja ya majimbo yatakayogawanywa. Watawindana kuhakikisha kila moja anagombea jimbo tofauti na huenda wote wakawa wabunge
 
Shida amezubaa halaf ali invest katika kutembelea viugomvi vidogo vidogo wakati arusha ilitaka kiongozi.
Hata hivyo wamemvumlia sana
 
Ili akapate nini huko?
 
Hii itakuwa move mbaya sana kwake, akomae huko huko CCM
 
Waanzilishi wengi kwa mazingira halisi wangetoka ccm wakati huo, kwani nchi ilikuwa ya chama kimoja. Hivyo wakati ule ndio ilikuwa uhalisia. Lakini haina mahusiano na ulichoquote toka kwangu.
Hata kwa sasa Chadema ni plan B ya wale wana CCM wasiomtaka Samia
 
Aliekuwa boss wake ambae kwa sasa ni marehemu hayupo hivyo saa hivi gambos hana makali tena ndio maana kabaki mnyonge kam 7ya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…