Msaada: Aliyeniuzia kiwanja kakiuza tena kwa mtu mwingine

Msaada: Aliyeniuzia kiwanja kakiuza tena kwa mtu mwingine

Kitumburee

Senior Member
Joined
Jan 31, 2012
Posts
142
Reaction score
88
Habari zenu wana jamvi, naomba msaada wa kisheria.

Nilinunua eneo Mabwe pande, eneo linaitwa Kinondo kijiji cha Utulivu mwaka 2017. Eneo hili lina documents za serikali ya mtaa ila halina hati. Tangu muda huo nimekuwa nikilima mihogo na nimeweka alama za mipaka katika eneo langu.

Cha kushangaza nilienda wiki mbili zilizopita nikakuta mtu anajenga hapo akidai kuwa ameuziwa eneo hilo na ana hadi documents za serikali ya mtaa. Nikamshtaki polisi, nikaenda kwa Mwenyekiti wa Mtaa kutoa taarifa na Ofisi ya Mtendaji pia, Mtendaji akaandika katika hilo jengo kuwa ujenzi usimamishwe. Cha kushangaza yale maandishi yamefutwa na ujenzi unaendelea.

Muuzaji ndiyo yule yule aliyeniuzia mimi na kwa sasa amekimbia. Kamati ya usulihishi ya kijiji haina msaada wowote kwangu kwa sababu hiyo hiyo kamati ndio ilihusika katika hayo mauzo ya huyu jamaa.

Naombeni ushauri nifanye nini?

Eneo hilo watu wengi sana wamedhulumiwa viwanja vyao na jamaa mmoja anaitwa Imma ambae yumo katika hii kamati ya usuluhishi. Majirani zangu wanadai waliogopa kunishtua walivyoona eneo linauzwa kwa kumuogopa huyo Imma kwa sababu anawatishia maisha yao.

Kamati hii ya usuluhishi haina msaada kwa kigezo kwamba aliyejenga ndio atapewa kiwanja haijalishi ameuziwa lini.

Naombeni ushauri nifanye nini.
 
Pole sana mkuu, kama hutopata solution ya jambo hili naomba utafute wakili yeyote karibu nawe akupe muongozo wa kishelia
 
Pole saaana! Hadhi ya eneo la ardhi kiumiliki linaanzia shamba, kiwanja, nyumba, hati miliki. Wewe ulikuwa unamiliki kiwanja na ilikuwa ni wajibu wako kukilinda kwa kuweka waangalizi au kukiendeleza kwa kukijenga ama kuweka msingi au kijumba cha kiaina kuzuia au kuonyesha eneo hilo tayari lina mmiliki. Watu wengi wenye mashamba na viwanja ambavyo havijaendelezwa hufanya hivyo. Vinginevyo mtu akija akajenga ina maana kakiendeleza hivyo mkienda kishitakiana ukadhibitisha ulikimiliki kabla yake, kiungwana utarudishiwa hela yako. Tukumbuke kuendeleza sehemu tunazomiliki au tuweke watu wa kutuangalizia. Wengine humwaga mawe, mchanga au matofari. Hata hivyo itakubidi umtafute aliyekuuzia ili kuweka msisitizo
 
Mambo matatu,
1.Mtafute Muheshimiwa lukuvi
2.Mwambie imma.serikaki siyo Mali yake binafsi akurudishie Eneo lako asije kukulaumu Baadaye mambo yakiwa makubwa.
3.Jenga Nyumba yako hapo hapo na wewe, akibomoa yako bomoa yake. We Jenga hapohapo hata kwa kukopa ukweli utajulikana Huko mbeleni
 
Pole saaana! Hadhi ya eneo la ardhi kiumiliki linaanzia shamba, kiwanja, nyumba, hati miliki. Wewe ulikuwa unamiliki kiwanja na ilikuwa ni wajibu wako kukilinda kwa kuweka waangalizi au kukiendeleza kwa kukijenga ama kuweka msingi au kijumba cha kiaina kuzuia au kuonyesha eneo hilo tayari lina mmiliki. Watu wengi wenye mashamba na viwanja ambavyo havijaendelezwa hufanya hivyo. Vinginevyo mtu akija akajenga ina maana kakiendeleza hivyo mkienda kishitakiana ukadhibitisha ulikimiliki kabla yake, kiungwana utarudishiwa hela yako. Tukumbuke kuendeleza sehemu tunazomiliki au tuweke watu wa kutuangalizia. Wengine humwaga mawe, mchanga au matofari. Hata hivyo itakubidi umtafute aliyekuuzia ili kuweka msisitizo
ndio inakua hivyo? kulima pia hakuhesabiwi kama kuendeleza maana pana mihogo yangu hapo.
halafu inakuaje kama na mimi nikijenga hapo hapo maana kiwanja ni kikubwa
 
Ni kweli kulima ni ishara ya umiliki lakini ni rahisi kufutwa na anayetaka kuuza kwa kusema alikuwa analimalima tu. Ujaona mtu anajenga nyumba hajamaliza au hajaamia anaandika kwa maandishi makubwa: NYUMBA HII AIUZWI OGOPA MATAPELI". Hakuna mnunuzi anaweza kuuziwa hivyo nyumba/pagale/kiwanja hata matapeli wanaogopa.
Kwa suala lako itabidi kwanza umtafute aliyekuuzia kwanza. Kisheria ni hivi: Nyoote mlinunua ardhi aijaendelezwa. Kama na yeye asingeiendeleza, wewe uliyetangulia kununua ndo mwenye hiyo ardhi na huyo wa pili katapeliwa. Kama huyu wa pili kajenga bila wewe kwenda mahakamani au hata polisi au hata wewe kwenda pale ungezuia (mtu ataanzaje kujenga eneo langu kwa mfano????). Vinginevyo unaonekana ni uzembe wa kushindwa kulinda mali yako! Anyway pesa yako utarudishiwa hopefully na gharama za kesi na fidia na atakayelipa ni huyo tapeli. Cha muhimu mtafute lakini kurudishiwa kiwanja/shamba ni ngumu au nenda kwa sangoma; ndo maana viwanja na nyumba zinaongoza kwa mazingaombwe
 
Ni kweli kulima ni ishara ya umiliki lakini ni rahisi kufutwa na anayetaka kuuza kwa kusema alikuwa analimalima tu. Ujaona mtu anajenga nyumba hajamaliza au hajaamia anaandika kwa maandishi makubwa: NYUMBA HII AIUZWI OGOPA MATAPELI". Hakuna mnunuzi anaweza kuuziwa hivyo nyumba/pagale/kiwanja hata matapeli wanaogopa.
Kwa suala lako itabidi kwanza umtafute aliyekuuzia kwanza. Kisheria ni hivi: Nyoote mlinunua ardhi aijaendelezwa. Kama na yeye asingeiendeleza, wewe uliyetangulia kununua ndo mwenye hiyo ardhi na huyo wa pili katapeliwa. Kama huyu wa pili kajenga bila wewe kwenda mahakamani au hata polisi au hata wewe kwenda pale ungezuia (mtu ataanzaje kujenga eneo langu kwa mfano????). Vinginevyo unaonekana ni uzembe wa kushindwa kulinda mali yako! Anyway pesa yako utarudishiwa hopefully na gharama za kesi na fidia na atakayelipa ni huyo tapeli. Cha muhimu mtafute lakini kurudishiwa kiwanja/shamba ni ngumu au nenda kwa sangoma; ndo maana viwanja na nyumba zinaongoza kwa mazingaombwe
shukran mkuu kwa ushauri
 
Back
Top Bottom