Msaada Biashara ya Library

Joined
Jan 26, 2013
Posts
6
Reaction score
2
Wadau nimekuja hapa kwenu JF najua hamna kinachoharibika maana meng hutatutuliwa humu nahitaji kufungua library ya kukodisha mikanda ila nahitaji iwe ya kisheria zaid nauliza kunataratibu zozote zile zinafanyika kwa wenye mamlaka na Bongo movies kuzikodisha?

Yaan kama ukataji wa kibali naombeni msaada wa hili jambo na kama kukata kibali naomba maelekezo wapi wanakatia na gharama ni shilingi ngapi?
 
Nilifikiri ni library ya vitabu, ningekwambia andika maumivu.
 
Watanzania ni wavivu sana KUSOMA ndo maana hata tukienda kwenye interview ukiulizwa la General tu jasho linakutoka hatari
 
Lol! Inaitwa Digital library au?
 
Wadau sijapata jibu bado nahitajika nipate kibali Cosota au kuna chama chochote kinatoa kibal kwa ajil ya kukodisha cd za movie za Kitanzania?Kama kuna mdau anajua hili anisaidie maana ninakahela kangu kangama nataka nikaingize hapo na nishaanza kukadokoa kasiishe bure mdau ajitokeze nami niweze kujikwamua kwa kuwakodisha cd hz maana naona library ni nyng kila eneo
 
Nadhani kwanza uende TRA ukarekebishe mambo yao, pili kama utakua unauza CD original na sio fake pia kama ukiwa haufanyi issue ya ku-burn CD sidhani kama ni tatizo unaweza anza bila ya kwenda COSOTA, ila kama una wasiwasi COSOTA ndo wanapotoa vibari kuhusu haki za wasanii, ni biashara nzuri kama utapata sehemu nzuri, isiwe Uswazi sana wala isiwe kwa kishua sana, pia iwe sehemu yenye movement ya kutosha yenye Wakazi na wapita njia cuz utakua unakodisha pia kuuza, uzuri ni kuwa ukiwa na Mil. 1 mpaka 1.5 unafungua Library ya ukweli na itakulipa brother.
 

Nenda basata
 
Shukran mkuu ubarikiwe sana nitafanyia kazi hii
 
Humu ndani kuna wasanii wengi, ni kweli hamjui taratibu za kufanya biashara ya kukodisha na kuuza Bongo movies? Wasiliana na Joyce Kiria atakupa data zaidi.
 
Habarin Wadau,nko Ruvuma Huko Nataka Kuanzsha Biashara Ya Kukodisha Na Kuuza Kanda Za Cd,vp Ina Athar Gan Hii Biashara?na Je Kwa Sh.laki Tano Itatosha?
 
Habarin Wadau,nko Ruvuma Huko Nataka Kuanzsha Biashara Ya Kukodisha Na Kuuza Kanda Za Cd,vp Ina Athar Gan Hii Biashara?na Je Kwa Sh.laki Tano Itatosha?

hivi kuna kanda za cd kweli?,andika vizuri ueleweke usaidiwe mzee,inawezekana ukawa umewaacha njia panda wachangiaji wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…