MSAADA: BRO WANGU ANATUMiA MADAWA

GAMBLER

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2009
Posts
303
Reaction score
11
Habari zenu wanajamvi
Nina kaka yangu ambaye amerudi Dar kutoka Ulaya alipokuwa anaishi, sasa sisi hatufahamu kama anatumia madawa ya kulevya, ameanza kuumwa na kutetemeka na anafanya fujo sana ili apate hayo madawa yake.
nilikuwa naomba msaada wenu, wapi tunaweza kumpeleka apate matibabu ya uhakika

 
pole sana mkuu, nimesikia MOMBASA kuna hospita nzuri sana lakini sina uhakika sana, labda subiri majibu utapata tu
 
Pole ndugu, mimi pia nina tatizo kama lako. Niliingia humu jamvini nikapata ushauri na maelekezo: Jaribu Muhimbili psychiatric unit, au Tanga (Lutindi Mental Hospital), au Mombasa.
Kwa bahati mbaya bado sijafanikiwa kwani anaendelea kutumia. Labda Kaka yako hajafikia chronic stage, anaweza akafanikiwa kuacha. Nashauri Lutindi ndio panasifika sana.
 
thanx mkuu
 
Kuna clinic karibu na aga khan
pia aga khan jaribu huko

huko ulaya alipotoka ndio kwenye matibabu zaidi

vyovyote vile ni mpaka yeye mwenyewe aamue kuacha
vinginevyo kazi bure.......
 
ushauri wa bure,mtu hawezi kuacha kutumia hayo madawa bila kutaka.Tumieni nguvu ,kutetemeka ni dalili ya dawa kuisha mwilini[wthdraw syndrome],hivyo atakuwa anafujo ile mbaya.Cha kufanya.kaongeeni na polisi,kisha awekwe ndani,hata kwa wiki tatu,halafu baadaye mtoeni.Hiyo sumu itakuwa imeisha.baada ya hapo muanze matibabu ya kisaikolojia.msisahau kumpeleka kwa wala unga chronic awaone walivyochoka.hapo atapata tafsiri ya wapi alikuwa anaelekea.
 
mpeleke korogwe tanga kuna hospital nzuri sana.kwa yote pole sana
 
sumu ya teja ni segerea mpelekeni fasta apone
 
Tatizo la unga ni kubwa sana... hapa Tanzania nafikiri wataalamu wapo ila ni wachahe na hawajawezeshwa... au tuseme hakuna kitengo maalum cha rehabilitation

Wanaoshauri apelekwe segerea sidhani kama ni suluhisho, maana makao makuu ya illicit drugs ni huko magerezani... atauza utu ili "apone"

Mpelekeni hospitali, kama walivyoshauri wadau hapo juu, anza na Muhimbili, pale utapata ushauri nini cha kufanya the muendelee huko Tanga na Mombasa...

All in all, tunamuweka kwenye Maombi
 
Mpeleke kwa pusha akajidunge, atapona.
 

Attachments

  • Unga.jpg
    108.7 KB · Views: 151

Kumpeleka Polisi ni jambo la hatari sana, huyu si mhalifu bali anasumbuliwa sana na Withdraw syndrome kwasababu alishakuwa dependant.
Hili ni tatizo linalohitaji kitu kinaitwa Rehabilitation na baada ya muda mtu anakuwa sawa. Rehabilitation kwa kiswahili kisicho rasmi ni ukarabati kwa maana kumrudisha katika hali yake. Kwa taarifa matibabu ya mtumia madawa ya kulevya ni dawa za kulevya! Tofauti ni kuwa anapewa dozi ndogo na kwa mpangilio ikipunguzwa kidogo kidogo hadi mwili uzooee kukaa bila dawa za kulevya. Tanzania tuna Psychaitry ward hatuna rehab centres kwahiyo mpeleke Muhimbili au kama walivyosema wengine Lutindi, Mirembe, Bugando n.k.
 
Mpeleke kwa pusha akajidunge, atapona.

Great thinker hilo!...tujaribuni kuwa serious wakati mwingine haswa kwenye swala sensiitive kama hili.Sio lazima u-comment kila post.
Take a minute to think deeply about the situation mtoa mada aliyonayo....sad!
 
Nafikiri Rutindi ni mwafaka zaidi ya Muhimbili.
 
afadhali hata nimeiona hii maana hata mdogo wangu anasumbua ivo ivo yani, huu ushauri nitaufanyia kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…