Msaada! dawa ya kukausha kidonda cha mwili

Chizy Za kitaa

Senior Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
167
Reaction score
13
Jaman mimi nina kidonda cha zaidi ya miez mitatu. Naombeni mniambie ni dawa gani nitumie ili kidonda changu kiweze kukauka kabisa pamoja na gharama zake?
 
NEEDS TO BE EVALUATED AND TREATED BY A QUALFIED MEDICAL DOCTOR.

MBADALA:

KAMA NI SEPTIC WOUND, OSHA na H2O2 ;WEKA IODINE TINCTURE; COVER WITH STERILE COTTON WOOL- KILA SIKU MPAKA KIPONE.
 
pole ni kidonda cha wapi? mi siyo doctor na wala sina utaalamu kabisa kwenye sekta hiyo ila mimi nilisumbuliwa na kidonda cha operation nilitumia zinc ya gnld, kwa sasa sijui wanauza ngapi ni linunua hapo imalaseko posta na kiukweli kidonda kilikauka haraka, na ieleweke sijafanya promo ya dawa kwani siyo shabiki wa hizo biashara ila ilinisaidia sana.
 
Reactions: BAK
Nenda hospitali. Inaweza kuwa sio kidonda tu cha kawaida. Kilianza vipi?
 

Hata mm kinansumbua kdonda cha operation,,kwan we enzi hzo ulinunua sh ngap?
 
NEEDS TO BE EVALUATED AND TREATED BY A QUALFIED MEDICAL DOCTOR.

MBADALA:

KAMA NI SEPTIC WOUND, OSHA na H2O2 ;WEKA IODINE TINCTURE; COVER WITH STERILE COTTON WOOL- KILA SIKU MPAKA KIPONE.

Thanks doctor
 
Najua sio mahali pake lakini nichuka nafasi hii kulizungumzia hili kidogo, kuna mtindo umezuka wa wadada wa mjini kupenda kuchagua kujifungua kwa operation badala ya njia ya kawaida hii ni mojawapoya complication ambazo ni common sana kutokea pamoja na maumivu ya tumbo yasiyoisha. Kwa hiyo kama hujashindwa kujifungua kwa njia ya kawaida nashauri usikimbilie upasuaji. Na madaktari wanaodanganya wagonjwa kuwa kujifungua kawaida mtoto anakua na risk ya birth injuries nadhani ukweli wake ni mdogo sana kama kutakuwa na usimamizi wa kutosha. Mara nyingi kama ni rafiki au wamevuta mshiko wanapenda caessarean section kwa kuwa ni rahisi sana kwao.

Back to the topic ni kwamba mara nyingi kidonda kinagoma kupona kwa kuwa kimepata maambukizo ya vijidudu na hivyo vijidudu vinasababisha ile tissue iliyokuwa inatakiwa iunge inalika na kushindwa kuunga. Inatakiwa kidonda hicho kiangaliwe na mtaalamu kuweza kuja ni kwa nini hakiponi na ukubwa wa tatizo ili kuweza kukupa matibabu sahihi kuendana na tatizo lako. Ni kosa kubwa sana kwa daktari kutibu mtu anayeeleza tatizo kwenye simu maana unaweza ukafikiri ni kubwa sana kumbe ni dogo au ukadhani ni dogo kumbe ni kubwa kwa kuwa kila mtu anaangalia vitu kwa mawazo tofauti kidonda mzaramo atakacokuambia kikubwa mkurya atakuambia ka kidonda kadogo tu. Baada ya kuandika saaana ushauri wangu ni kionwe na mtaalamu hasa daktari aliyekufanyia hiyo operation atakuwa na ushauri zaidi. Nikutakie siku njema na ugia pole...
 
Aisee wahi hospitali fasta. Kidonda cha upasuaji cha muda mrefu hivyo hakiponi kwa sababu ya maambukizi kama ulivyoelezwa hapo juu. Kitahitaji kukwanguliwa tissue zilizokufa, kufungwa kwa usafi wa hali ya juu na very strong antibiotics.

NENDA MJINI HOSPITALI HARAKA
Kidonda cha upasuaj ndugu!
 
Pole sana kwani hosp wanasemaje ulikopasuliwa? ila pia check vitu kana sukari mwilini huchelewesha kidonda kupona. Kwa imani huna ila check tu.

Asante kwa ushaur,,hosptal ipo mjn mm nipo kjjn
 

nashukuru kwa ushaur
 
jaman mm nina kidonda cha zaid ya miez m3.. Naomben mniambie ni dawa gan nitumie ili kidonda changu kiweze kukauka kabisa pamoja na gharama zake?
Mkuu Chizy Za kitaa

DAWA YA KIDONDA SUGU :

Pakaa Asali kila siku kwenye kidonda chako utapona.


ASALI DAWA YA VIDONDA
Tangu enzi na enzi, asali imekuwa ikitumiwa na mababu zetu kama chanzo cha nishati ya mwili, lakini pia katika utafiti wa hivi karibuni, imegundulika kuwa asali ina ewezo mkubwa sana wa kuponya vidonda vya aina mbalimbali kutokana na viambata vyake kuwa na uwezo wa kukausha maji haraka kwenye kidonda.

Aidha, virubisho vingine vilivyomo kwenye asali vina faida kubwa kwa wana michezo kwani huongeza nguvu na wana michezo wengi wamekuwa wakitumia vyakula vitokanavyo na asali au vyenye mchanganyiko wa asali na wameona mafanikio makubwa.
 

Attachments

  • asalii.jpg
    12.1 KB · Views: 624
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…