Msaada: Elimu na ushauri kuhusu SACCOS

melech

Member
Joined
May 29, 2013
Posts
62
Reaction score
25
Amani kwenu wote!

Nafikiria kujiunga na SACCOS mojawapo ila kabla sijafanya hivyo, ningependa kupata elimu kidogo kuhusu SACCOS. Pia napenda kufahamu ni vigezo gani vya kuzingatia katika kuchagua SACCOS ya kujiunga ili niweze kupata faida za kujiunga na SACCOS.

Najua mle watu wanaweka pesa zao na kukopa, ila taratibu zake huwa zipoje? Hapa niangalie nini wakati nachagua moja ya kujiunga?
Ni vipi viashiria vya hatari katika SACCOS yoyote? Nitavigunduaje? (bila shaka kwa swali hili nitafahamu viashiria ya mafanikio pia). Masharti yake ni yapi?

Na jambo lolote la kufahamu na kuzingatia kuhusu SACCOS tafadhali. Napenda kusikia kutoka kwa walio wanachama wa SACCOS.

Duh, nime-search hapa JF kwa keyword "SACCOS" yamekuja mambo ya vyama vya siasa na wanasiasa tuu!(jaribu ku-search uone) Sijui vipi!!

Asanteni.
 
Mojawapo Kigezo cha kujua kuwa SACCOS unayotaka kujiunga nayo kuwa sustainable 'endelevu', ni kuwa na wanachama wengi 'hai' wanaopata huduma. SACCOS yenye wanachama wengi hai kwa kawaida lazima hata mtaji wake utakuwa ni mkubwa kwa kuwa watu watakuwa wanafanya savings kwa kiasi kikubwa na watakuwa wanakopa kwa kiasi kikubwa pia,hivyo SACCOS kupata kipato kikubwa kupitia riba inayopatikana kupitia marejesho wanayoyafanya.

Ukiona unaenda SACCOS unakuta kuna movement chache za wateja, lazima itakuwa haipo vizuri sana,ukiona unaenda SACCOS kutaka kukopa unaambiwa uje baada ya miezi miwili au zaidi,ujue hawana mtaji wa kutosha.

Taratibu za kuwa mwanachama ni kwenda kwenye Ofisi za SACCOS husika,watakupa taratibu zote ikiwemo kulipia kuwa mwanachama, kununua Hisa,n.k.

Ukitaka kukopa lazima uweke akiba na utakopeshwa si zaidi ya mara tatu ya akiba yako, Mfano Ukiwa na Akiba ya milioni moja, utakopesha milioni tatu kwa riba watakayokuelekeza na muda wa marejesho utakaoelekezwa,wengine wataongezea mkuu.
 
Steveachi,

Asante sana kwa mchango & uelimishaji wako. Nimesoma na nikaelewa uliyoandika yote. Nakushukuru tena kwa kutenga mda wako kuelimisha. Nadhani nitapata mchango zaidi kwa wadau wengine.

Asante na Kila la heri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…