Msaada-fidia ya kupata ugonjwa unaohusiana na kazi

Msaada-fidia ya kupata ugonjwa unaohusiana na kazi

moto2012

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2012
Posts
2,271
Reaction score
1,493
Dada yangu ni fundi sanifu maabara (Lab. technician) katika hospitali ya Wilaya X, miezi sita iliyopita aligundulika kuwa na TB, alitibiwa na kupona, baada ya hapo alichukua hatua ya kudai fidia ya kupata ugonjwa akiwa kazini. Alipomwandikia barua Mkuu wake kutaka fidia, alijibiwa kwa kuwa anaishi na VVU hawezi kulipwa fidia. Wadau naomba nisaidieni (hasa wajuzi wa occupational health na occupational laws), je ni kweli dada yangu hastahili fidia? Na kama ndio huo sio unyanyapaa?
 
Kama dada yako anaishi na VVU inawezekana TB yake haitokani na kazi yake bali ni ugonjwa nyemelezi kwa sababu immunity system yake ni dhaifu. Mtu anapata fidia kama madhara aliyopata yana uhusiano wa moja kwa moja kuwa yametokana na kazi anayofanya.
 
kama mdau alivyozungumza hapo juu, TB na HIV ni mtu na binamu yake. TB humtokea mtu pale kinga ya mwili inapokuwa imepungua. maana yake ni kuwa katika mazingira yetu haya, wengi wetu tunatembea ama tunaishi na vimelea vya TB, ila kwa kuwa kinga zetu zipo juu, tunafaidika kutopata ugonjwa huu. pale kinga ya mwili inapopungua, ndipo ugonjwa huu unajitokeza. Katika stages za WHO kuhusu watu wanaoishi na HIV/AIDS, mtu akipata TB anaonesha kuwa yuppo katika stage ya 3 ya kuishi na virusi.

Kwa hiyo ndugu yangu, hapo hakuna fidia. atumie dawa kama alivyoagizwa na daktari, hadi miezi hiyo yote iishe. Mungu atambariki
 
Back
Top Bottom