Msaada gari imegoma kuwaka ghafla

ECU ni ghali sana, kununua mpya bila kujiridhisha kuwa ni mbovu itakuwa ni hasara kubwa sana mkuu.
 
ECU ni ghali sana, kununua mpya bila kujiridhisha kuwa ni mbovu itakuwa ni hasara kubwa sana mkuu.
Anasema ilishaungua resistor moja; haiwezi kuungua bila sababu, na sababu hiyo haiwezi kuchagua resistor moja tu; kuna ICs ambazo pia zimeathirika. Njia rahisi kabla ya kuamua kununua ECU ni kufanya majaribio ya kutumia ECU nyingine ambayo inajulikana kuwa inafanya kazi.
 
Nadhani pendekezo lako kujaribu kutumia ECU ambayo inajulikana kuwa ni nzima ni zuri zaidi
 
Mkuu hiyo engine ya 2jz kama inasumbua nenda Geartech (GTP) pale hizo injini za 1jz, 2jz,Gc8,N12,N16 kila siku wanacheza nazo. Usiogope kaonane na mjapani atatatua tatizo bila ya kununua vifaa vipya.
 
Mafundi walitrace wire iloleta short wameipata na kuiondoa kwenye wire zilizopewa moto before putting ECU back. Nimeona nitafute ECU nyengine huenda ikawa ndio tatizo kama usemavyo.

ECU ni ya obd1 na i think inakuwa ghali kwa sababu ya upatikanaji wake kuwa mgumu.

Kuna mtu amenishauri kuweka wiring ya 1g kavu, maana zipo zipi izi pamoja na ECU yake. Sasa mimi sijakubaliana na hilo, 1G ni 2000cc na ni around 150HP, 2jzge ni 3000cc na ni 220HP, sasa nikitumia control ya 1G kavu perfoamnce si itaporomoka? au vipi?
 
Mkuu hiyo engine ya 2jz kama inasumbua nenda Geartech (GTP) pale hizo injini za 1jz, 2jz,Gc8,N12,N16 kila siku wanacheza nazo. Usiogope kaonane na mjapani atatatua tatizo bila ya kununua vifaa vipya.
Niko Zanzibar mkuu ndio shida yote hii 😀 ningekuwa Dar ningewaendea zamani tu mana najua wale jamaa wanacheza nazo sana.
 
Kabla ya kununua ECU, tafuta moja inayofanya kazi kwenye gari nyingine uijaribie kwenye gari yako kuona kama kuna tofauti. Solution ya tatizo lako inataka mtu kukagua sehemu mbalimbali za gari, lakini ukaguzi huo una maana tu kama ECU inafanya kazi sawasawa. Kama fundi wako ana computer inayoweza kusoma real time data, mwambie afanye hivyo mnaweza kukuta kuna namba fulani hazibadiliki kuonyesha ECU imekufa.
 
Sasa kuipata ECU, kuna mzee mmoja hatujuani na tunakaa mitaa tofauti ana baloon inayo 2jzge, ila sasa unajua watu wazee walivo, ukimwambia unataka utest ECU yako anaeza ona unataka kumbomolea na akakutolea nje 😀

Fundi amesema tujaribu kwa wiring na ECU ya 1G kavu, ikiwa haikati moto, basi tatizo ECU, ikiwa inakata basi Distributor itafutwe nyengine tu.

Vipi swala la kutumia wiring ya 1g kavu na ecu yake, perfomance ya engine itakuwa ki 1G au ita maintain perfoamnce ya 2jzge?
 
Niko Zanzibar mkuu ndio shida yote hii 😀 ningekuwa Dar ningewaendea zamani tu mana najua wale jamaa wanacheza nazo sana.

Mkuu jaribu kuwasiliana nao GTP kwa Instagram au mawasiliano. Jamaa wako poa sana kwa hizo injini watakupa msaada hata kwa njia ya siku au sms.

Pia mcheki Shayo STI Instagram atakusaidia hilo tatizo.
 
Mkuu jaribu kuwasiliana nao GTP kwa Instagram au mawasiliano. Jamaa wako poa sana kwa hizo injini watakupa msaada hata kwa njia ya siku au sms.

Pia mcheki Shayo STI Instagram atakusaidia hilo tatizo.
Nimepata reply from GTP wamenambia wiring itakuwa imekosewa nicheki diagram.

Sasa nimegoogle nimepata diagram ya Supra, ECU sawasawa lakini tatizo kuna pins kwa yangu zipo blank, yaani hakuna connection ya wire.
 
Nimepata reply from GTP wamenambia wiring itakuwa imekosewa nicheki diagram.

Sasa nimegoogle nimepata diagram ya Supra, ECU sawasawa lakini tatizo kuna pins kwa yangu zipo blank, yaani hakuna connection ya wire.
Sawa, jamaa wasiliana nao kila hatua na kama inawezekana mpe na video ukiwasha gari.

GTP kwa injini hizo hata iwe kwenye hali gani, wao kuirudisha kuwa kawaida wanaweza.
 
Mrejesho,

Nimenunua ECU nyengine, bahati nzuri sana mwenyewe amekubali niirudishe ikiwa haijanifaa. Nimeipachika hio ECU, yani hata engine haijawashwa, tukasema tuipime kwanza ECU ina cde gani, tukakuta in Code 12 RPM signal na Code 14. Tukajua kuwa haitowaka gari lakini tukasema tuombe Mungu, tukajaribu ndio ilikuwa inapiga chafya tu ngoma haiwaki. ECU ya zamani nikiweka moto mmoja tu inawaka sema ndio inakata. Tumeamua kuwa ECU sio Tatizo na nimerudisha.

Kilichonikwaza ni mafundi wangu, Walikuja wakanambia kuwa niwaongezee dau, wataiwasha gari kwa kutumia ECU hio hio na wiring hio hio! Ndani ya nafsi nikawa najisemea kuwa hawa tatizo wameshalijua, mda tu, ila wametaka hii kazi niione ngumu na nikubali kuwaongezea hela. Nikapatana nao kidogo, wakanambia watanijibu kesho.
 

Kwenye ufundi wa magari naona unajitahidi. Lakin kule kwenye vita ya Uganda aisee unabwatuka pumba tupu.
Nimeona jana na leo washikaji wamekuumbua kisenge
 

Kesho yake ikawaje?
 
0658300522, mcheki huyo dogo hautojutia
 
Kesho yake ikawaje?
Hakuna liwalo mkuu, walikuwa wamekariri kutoka kwenye engine nyengine sijui engine gani ambayo distributor yake ina waya 5. lengo lao ni kuchukua waya mmoja kutoka kwenye distributor na kuupa moto kupitia waya mwengine ili kuitrick ECU. Wakakuta distributor yangu ina waya 4 kwaio hakikuwezekana walichokuwa wanataka kukifanya. Nikatafuta wengine, kila mmoja ananambia nibadilishe wiring niweke ya 1gfe ilokuwa na distributor (yaani zile za zamani sio zenye vvti) nikaona watanirudisha nyuma hawa, utawekaje ECU ilotengezwa kufanya kazi na 2000CC ije ifanye kazi vizuri engine ya 3000cc. Nikahairisha na kuamua kurudisha mashine yangu ya mwanzo tu.
 
Kwenye ufundi wa magari naona unajitahidi. Lakin kule kwenye vita ya Uganda aisee unabwatuka pumba tupu.
Nimeona jana na leo washikaji wamekuumbua kisenge
Kama hunijui; mimi ni all weather kutokana na mazingira niliyokulia. Kila mchango wangu hapa JF huwa unatokana na ukweli kamili ninaojua kwa uhakika. Kwa watu wa aina yako ambao wanafahamu vita ile kwa kusimuliwa tu huwa wanachukulia mambo nusu nusu tu na kuhitimisha kutokana na unusu huo. Ninapoongelea vita ya Kagera ni kwa sababu naijua sawasawa, na vile vile nikiongelea mawasiliano ya anga ni kwa sababu nayajua vizuri kijeshi, na nikiongelea ufundi wa magari ni kwa sababu naujua vizuri siyo mdakizi kama watu wa aina yako.
 

Okey, tufanye usemayo yote ni kweli.

Sasa iweje kuna watu walikua kwenye hiyo vita, tena wengine mlikua kambi moja (na wewe ukakubali kabisa) juzi wakawa wanakuumbua wanasema vitu vingi unaandika uongo!

Tena wenzako wote wali-admit kabisa kuwa Uganda War ilikua inahasara kubwa kuliko faida.

Tena uongo mwingine mkubwa walikuumbua ni kwenye mahindi ya Yanga. Wewe umeng'ang'ania yalikuja kabla ya vita, wenzako wote (walikuepo wakat huo) wanasema yalikuja baada ya vita.

Acha kujifanya mjuaji wa vitu usivovijua eti ili upate popularity. Nakushauri ubaki kwenye ufundi wa magari tu.
 

Kwanza elewa kuwa mimi sikwenda vitani; nilikuwa makao makuu ya brigedi kitengo cha mawasiliano. Halafu watu wa aina yangu wengi ambao nilikuwa nao wakati huo ni ama majenerali leo au wameshastaafu utumishi jeshini. Watu wale hawawezi kukubaliana ni hizo pumba zinazoletwa na watu waliosimuliwa kuhusu vita ile. Eti tulikuwa wanyonge hadi jeshi la Uganda lilivyoasi ndipo tukapata nguvu, eti tulisaidwa na jeshi la msumbiji ndipo tukashinda; huo ni upuuzi mtupu. Mambo ya kima-mantiki ya watu wanaotaka kumpa credi kubwa sana Kiwelu kuhusu vita ile mimi ninayapinga outright.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…