Msaada haraka tafadhali kichwa kinanikosesha amani ya kuishi

Nilifanyiwa maombi sna lakini sijapata nafuu yoyote. Asante kwa ushauri

Mkuu;
Mbona umesema ulimaliza masomo kwa msaada wa Mungu? Mungu gani huyo akusaidie masomoni ashindwe kukuponya kaugonjwa ambako unaona JF kuna daktari wake??
Mkuu, Soma sana neno la Mungu, liamini, litendee kazi utashangaa yatakayo kutokea. Mk. 16 : 16 - 18. Ni wewe unaambiwa mkuu sio watu fulani sijui manabii au ma appostle. ni weye mwenyewe. Amini neno, litendee kazi kabla hujakata tamaa. Aliyekuwezesha kumaliza masomo yako atakumalizia na hilo tatizo lako.
 
Nami pia nlikua na tatizo la kichwa nimeumwa sana tangu 2007, nikaenda muhimbili nikawa nahudhuria clinic napewa dawa nikimeza kinatulia zikiisha kinaanza upya, kuna siku nmeamka naumwa kichwa mpaka macho yanatoa machozi tu nikaenda hospital ya macho nikapewa miwani naona kimetulia sasa....
Nenda kapime na macho
 
Ahsante Evelyn, nimepima macho mara kadhaa tena mpaka hospitali ya macho mvumi. ntapima tena kujiridhisha.
 
Mungu akuepushe na maradhi makubwa lakini kwa maelezo yako unaweza kuwa na tatizo kubwa.
Kwa ushauri nenda kafanye scan.
 
Ningekuwa na afya njema labda ningebishana kitu hapa na wewe japo sipendi jambo hilo lakini lengo langu ni kupata msaada. Usijali nimekuelewa na nashukuru kwa mawazo.
 
Nenda MOI watakupa ushauri baada ya x ray, harakia tafadhali
 
TMJ hospital [emoji541] inatoaga huduma ya CT scan. Nenda kajaribu.
Kumbe kizunguzungu kina uhusiano na kikohozi.
Tatizo lako nami pia linanisumbua ila sina maumivu.
 
TMJ hospital [emoji541] inatoaga huduma ya CT scan. Nenda kajaribu.
Kumbe kizunguzungu kina uhusiano na kikohozi.
Tatizo lako nami pia linanisumbua ila sina maumivu.
Ahsante kwa ushauri, makohozi na kizunguzungu ni miongoni mwa changamoto zinazoendana na kuumwa kichwa, nimehisi tu kuwa labda kuna uhusiano.
 
Ningekuwa na afya njema labda ningebishana kitu hapa na wewe japo sipendi jambo hilo lakini lengo langu ni kupata msaada. Usijali nimekuelewa na nashukuru kwa mawazo.

Aksante kama umenielewa ila dada bado niko pale pale kuwa, achana na kuwatafuta watu wa kukusaidia. Msaada wetu u katika BWANA aliyeziumba mbingu na nchi.
Ni yeye tu aliyethubutu kutuambia kuwa Mt. 11 : 28 Njoni kwangu ninyi nyote mnaosumbuka na kuelemewa na mizigo nami nitawapumzisha.
Mwendee huyo atakusaidia.
 
Pole sana kwa tatizo lako..
Katika maelezo yako umesema unasahau sahau..je unasahau sahau kwa jinsi/namna gani?
Mfn. MTU akikwambia kitu baada ya muda unasahau mpaka kakumbushe? Au unasahau majina ya vitu ambavyo ni vya kawaida kabisa mfn..Pencil, daftari na nk.?

Kuhusu kuumwa na kichwa, Kuumwa kichwa si ugonjwa Bali ni dalili za ugonjwa fulani.

Cha muhimu nenda Hospital/Daktari tena na tena kwani kuna magonjwa mengine yamejificha yanahitaji uchungunzi wa hali ya juu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…