JOTO LA MOTO
JF-Expert Member
- Apr 11, 2018
- 758
- 555
Kipindi nakuwa nilitokea kuwa mnazi kindakindaki wa timu ya Simba, ingawa kwa sasa sio kwa asilimia zile zile nilizokuwa nazo kipindi kile. Wakati ule nilitokea kuvutiwa na baadhi ya Majina ya Wachezaji kadhaa, hivyo basi ombi langu naomba yeyote mwenye taarifa walipo Jamaa hawa kwa sasa, na kama walishatangulia mbele ya haki basi Wapumzike kwa amani. Wachezaji hawa wafuatao:- Sunday Juma, Zuberi Magoha, Lila Shomari, Malota Soma, Ezekiel Grayson (Jujuman) huyu nilisikia baadae kwamba ndiye Baba wa Aunty Ezekiel, Kiwelu Musa, Moses Mkandawile, Ibrahim Marekano, Abdul Mashine, Daudi Salum (Bruce lee)...