Msaada: Hosp. Or clinic ya kupima afya

Msaada: Hosp. Or clinic ya kupima afya

Shoo Gap

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2009
Posts
261
Reaction score
97
Tafadhali naomba msaada wa kituo/clinic/hosp. inayotoa huduma ya kufanya vipimo vya afya kwa mtu asiye mgonjwa(just for check up). Nilienda hosp fulani nika line up kama mgonjwa nilipofika kwa Dr. akabaki ananishangaa tu baada ya kumwambia siumwi ila nimekuja kupima tu. Basi aliishia kuniambia nikatoe damu, mkojo n.k
 
sijajua ni kwanini baadhi ya hospital ukiwaambia unaenda for check-up wanakushangaa sana watakuambia pima damu na mkojo sijui ni kwanini?? ilihali tunaambiwa tucheck afya zetu.
 
Hospital nying tu ziko hivyo, ukisema nimekuja kufanya checkup wanakushangaa
 
Daktari alikushangaa maana umekaa kwenye foleni na kuzuia wagonjwa wengi waliokuwa mahututi, wale wa check up inabidi wawe na muda wao maalum, kumbuka madaktari ni wachache
Tafadhali naomba msaada wa kituo/clinic/hosp. inayotoa huduma ya kufanya vipimo vya afya kwa mtu asiye mgonjwa(just for check up). Nilienda hosp fulani nika line up kama mgonjwa nilipofika kwa Dr. akabaki ananishangaa tu baada ya kumwambia siumwi ila nimekuja kupima tu. Basi aliishia kuniambia nikatoe damu, mkojo n.k
 
Mokoyo sikukaa foleni bila kufanya reg, pale mapokezi ndo walinielekeza nikae foleni na wagonjwa. Nilitegemea kila hosp kuwa na kitengo & specialist wa check up. Bado sijapata jibu na ninamaanisha kupata Dr mwenye uelewa nini maana ya check up.
 
Last edited by a moderator:
Naona utaratibu wa kupima afya kila mara ili kuyawahi magonjwa hakupewi nafasi kubwa - shida ni upungufu mkubwa wa madaktari katika mfumo wa afya wa serikali. Hata hivyo baadhi ya hospitali binafsi zina utaratibu wa uchunguzi detailed japo kwa gharama kubwa.
 
Mkuu Shoo Gap,

'Check up'...esp. Full body check up ni (Body scan kuangalia magonjwa au uwezekano wa magonjwa) na tunaisistiza angalau mara moja kwa miezi mitatu.Hii tukimaanisha uchunguzi wa afya kufanyika kwa karibu kila kiungo.

Mwilini kuna baadhi ya sample tunazozitumia kuangalia vitu/mambo mbali mbali katika kuangalia, kuchunguza, kufuatilia/kuangalia maendeleo ya mgonjwa(patient) au client(iwapo haumwi).

Ikumbukwe wengi wa watu wanaokwenda hospitalini huenda kama Patients na siyo Clients.


Sasa katika mwili wa binadamu tunaweza kuangalia haya yafuatayo(HAYA ni BAADHI TU.)

Damu:
-Kundi la damu,
-Sukari
-Madini(Na, K, Ca, Cl)
-Wingi wa damu
-Chembe chembe za damu, nyeupe, sahani n.k
-Urea
-Creatinine
-Mafuta yaliyo mwilini(Lipid Profile)
-Homa ya ini(Hepatitis Panel)
-VVU

Mkojo:
-Sukari
-Chembe za damu (nyeupe, nyekundu)
-Protini

Choo:
-Mayai ya minyoo
-Damu

CSF:
-Protini
-Chembe nyeupe za damu

Upigaji picha:
-Picha ya kifua((X-ray)/ CXR
-Picha ya moyo(ECG, ECHO)
-Uchunguzi wa masikio, pua na kinywa.


Kwa wanawake kuna vitu vingine kama;
- Abd-Pelvic USS/ Obstetric USS
- Pap smear n.k

Kila kipimo kina gharama yake, na hivyo basi watu kusita kufanya vipimo hivyo, Sasa ni jukumu la daktari wakati fulani kwa kutumia elimu yake kuangalia vipimo vipi avipe vipaumbele kuliko vingine, na hivyo basi SIJAONA kosa hata kidogo pale daktari alipokuambia ukatoe damu, mkojo n.k.
 
Last edited by a moderator:
Hippocratessocrates nashukuru sana kwa kunifungua macho kwa kina kuhusu aina ya vipimo ninacyoweza kufanyiwa. Ni wapi kwa DSM naweza kupata hii huduma ya check up?
 
Hippocratessocrates nashukuru sana kwa kunifungua macho kwa kina kuhusu aina ya vipimo ninacyoweza kufanyiwa. Ni wapi kwa DSM naweza kupata hii huduma ya check up?

Karibu na niwie radhi kwa kuchelewa kujibu.Hapa Dar es Salaam unaweza kuja Muhimbili lakini hapa itabidi kuja kama Private patient/client. Vile vile hospitali za wilaya hapa DSM (ingawaje neglect inaweza kujitokeza kwa kuwa daktari atahitaji kuona wagonjwa walio katika critical condition clinically(serious) kabla ya kukuona).

Kama uwezo ni mzuri hospitali binafsi ni sehemu bora mf. Regency, Aga Khan, TMJ pamoja na new Diahnostic centres zilizofunguliwa hapa mjini.

Baada ya vipimo hivi vya kwanza, yaani establishing Baseline profile, ni utaendelea kuangalia vipimo vya kawaida mf. Urefu, Uzito, Blood Pressure, Macho, n.k ili kuangalia maendeleo yako...vipimo vingine vitatokana na hali/uhitaji wako wa kiafya.

Iwe changamoto kwa wananchi wengine kuiga mfano huu.
Goodluck.
 
hippocratessocrates nashukuru sana kwa very satisfying info. Nitafanya jitihada kutafuta Hosp. moja private kisha ntawapa feedback.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom