Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hello Rangoo,
Wewe ni jinsia gani na una umri gani, kazi?
-Maumivu ya tumbo yako kwa muda gani?
-Maumivu ya tumbo yanakuwa eneo gani la tumbo(juu ya kitovu kulia/kushoto?chini ya kitovu kushoto/kulia?
-Je maumivu haya yanauma yakielekea upande/sehemu yeyote?
-Toka tatizo lianze umewahi kudondoka?Kuhisi kuchoka, au kuhisi mapigo ya moyo?
Je, umewahi kutumia pombe?(kama ndiyo, kwa muda gani na pombe kiasi gani kwa wiki?
Vipi kuhusu uvutaji wa sigara?
Je una ugonjwa wowote wa muda mrefu, pengine kukufanya utumie dawa za maumivu kila mara?
Kuna ndugu yeyote(upande wa Baba au mama wako aliyewahi kuambiwa/kugundulika ana tatizo la vidonda vya tumbo," Ulcers"?
-Kuna dawa zozote unazozitumia sasa?
Mi ni 20's..... Na male, maumivu ya tumbo yana mda wa siku mbili na nusu..., na ni ya eneo la katikati ya kitovu kushuka chini....
Toka tatizo lianze sijawahi dondoka, kuhisi kuchoka wala mapigo ya moyo,
situmii pombe wala sigara, nilipima miezi miwili iliyopita nilikuwa nasumbuliwa na minyoo ambayo pia ilikuwa inasababisha tumbo kuuma, nikatumia dawa tatizo likaisha..
Sasa hili ndo limeanza siku hii ya pili na nusu...Kwa ndugu kwa kweli siwezi jua wa upande wowote mwenye ulcers....
Kwa sasa situmii dawa ya aina yoyote ile... Ila nilikuwa nataka kutumia hivyo vitunguu swaumu nikidhan ni minyoo tena
Chakula pia nahisi kinaweza changia... Maana ni Maharage kwa sana.. Kishule shule
ASANTE