Msaada Jamani

cute beiby

Senior Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
129
Reaction score
44
Wakubwa shikamo, wadogo habari zenu !


Nilikuwa naomba kufahamishwa hivi kama umeolewa ndoa ya kiislam kutokana na sababu zisizo zuirika inabidi kutengana , taratibu gani zinabidi kufuatwa ??

Na hatuna watoto ila ni mjamzito.

Na vipi kuhusu kugawana mali inakuwaje?

Matunzo ya mtoto je?

Huwa inachukua muda gani?

Naombeni msaada wenu maana mambo yamekuwa magumu sana.
 
Sikushauri kudai talaka haraka haraka. Vumilia kwanza lakini kwa hali yako lazima muachane kwa mujibu wa sheria ZA kiislam na hata mgawanyo wa Mali ni kwa sheria hizo hizo, amabzo wengi wao huziona kua kandamizi kwa wanawake, jiyahf kua mvumilivu labda mambo yatakua sawia.
 
hapo utaondoka tu na begi lako la rambo na talaka tatu mengine huna chako hapo
 
cute beiby
Hapo kama unataka ndoa ivunjwe usipitie kwenye taratibu za dini maana hapo hutaitajika kupewa talaka tena tatu! Huwa ni ngumu kuvunja ndoa kwa kupitia taratibu za dini!

Hivyo basi unaweza kwenda ustawi wa jamii hapo utakuta kuna mabaraza ya usuluhishi na ni lazima kabla ndoa haijavunjwa lazima wajirizishe na hapo kwanza watasuluhisha pande zote mbili (mume na mke) mpaka wajilizishe kuwa hii ndoa imeshindikana kabisa ndio wa takupa go ahed ku file for divorce!

Hapa lazima ukumbuke ni lazima uwe na sababu za msingi kabisa za kutaka kuvunjwa kwa ndoa.

Lazima pia ukumbuke lengo la haya mabaraza ni kuhakikisha ndoa zina dumu na hazivunjwi kwa lazima ushawishi na ujiandae kwa sababu za kutosha!

Kuhusu malezi ya mtoto hata ukiachana na baba wa mtoto atakuwa na jukumu la kutoa matunzo ya mtoto na kuna utaratibu kabisa japo kisheria ni pesa ndogo sio zaidi ya elfu 15per moth if am not mistaken!

Kuhusu swala la mali kama ulichagua kulipeleka hili swala ki serikali basi kama mlichangia mali mtagawana na kama hukuwa na mchango wowote huto pata chochote! Na kama mumeo alikupa zawadi yeyote kama gari au nyumba na akakuandikisha basi itahesabika ni ya kwako!

Na kushauri kabla ujachukua huamuzi wa kuvunja ndoa ni vyema mka kaa na mumeo kuyamaliza maana furaha yetu ni kuona ndoa hazivunjwi bali zina dumu!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kawaida mahakama pekee ndio ina mamlaka ya kusema ndoa imevunjika na kimsingi mahakama haivunji ndoa ila inatamka (declare) kuwa ndoa imevunjika. Na kuna sababu zilizotajwa na Sheria ya Ndoa zinazoweza kusababisha ndoa ivunjike.

Kwahiyo kama ungesema wewe na mwenzako mna shida gani, tungeweza kukushauri. Hatahivyo suala la mgawanyo wa mali haliangalii kuwa una watoto au hauna, kinachoangaliwa ni mchango wako katika kupata mali mliyokuwa nayo na haijalishi kama wewe ulikuwa unafanya kazi au la kwani katika kesi ya Bi Hawa Mohamed, mahakama ilisema hata mama wa nyumbani anastahili kupata mgao wa mali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…