Msaada jamani

manking

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2014
Posts
1,306
Reaction score
316
Habari wana jamii,
kwa muda kama wa mwezi hivi nakuwa kama nimepaliwa na kitu bila hata yakula chochote wala kunywa ni(hewa tu)
hii inanipelekea kukohoa na kupoteza sauti kwa kama dakika moja. Hali hii inajirudia mara kwa mara. nimetumia dawa kama vile, mucolin, amoxylin na elythromycin sijaona mabadiliko.
Wenye uzoefu naombeni kujua ninatatizo gani na dawa yake ni nini. Ahsanteni.
 
Pole na changamoto.

Kutokana na maelezo yako ni kuwa sphincter iliyo kati ya esophagus na stomach haifanyi kazi sawasawa.

Hali hiyo inaweza kusababishwa na vitu vingi pamoja na matatizo ya ubongo, infection, hernia ya esophagus, uvimbe tumboni.

Iwapo hali hiyo itaendelea miaka mingi, inaweza kubadili tabia ya ukuta wa esophagus ambao haujazoea kugusana na asidi ya tumboni, jambo linaloweza kusababisha kansa.

Cha kufanya: hali yako inaweza kuwa serious zaidi ya unavyodhani. Ni vema ukaonwa na daktari wa magonjwa ya tumbo (gastroenterologist) ili atathmini ukubwa wa tatizo na kupanga matibabu.

Again, pole na changamoto.
 

Nashukuru mkuu ushauri wako nitaufanyia kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…