Msaada: Jinsi ya kuwa wakala M-Pesa, Tigo-Pesa na airtel money

gspace

Member
Joined
Nov 18, 2014
Posts
54
Reaction score
13
Wadau nataka kuwa wakala wa tigo pesa,m pesa na airtel money + luku . Lakini sijui nifanyeje ili nipate line hizo mwenye kujua anisaidie.
 
Wadau nataka kuwa wakala wa tigo pesa,m pesa na airtel money + luku . Lakini sijui nifanyeje ili nipate line hizo mwenye kujua anisaidie.

Kuna namna mbili za kuwa wakala.

Namna ya kwanza:
Unaweza kununua laini ya uwakala kutoka kwa mtu na ukapata details za muhimu kuhusu hiyo laini na ukaweza pesa yako ukaanza kazi.

Faida ya kununua laini iliyokamilika: ni njia rahisi ya kupata laini.
Hasara: laini hua ni ghari kidogo, lakini pia ikipotea itakupa shida sana kurenew maana hauna vitu muhimu vilivyotumika kuisajili hiyo laini kama leseni na TIN ya TRA.
Vile vile laini hii inaweza kua na jina la mtu mwingine (hii isikusumbue kichwa maana unaweza kubadilisha jina kua lako).

Namna ya pili:
Unaenda office za TRA huko ilipo, wambie unataka Taxpayer Identification Number yaani TIN, utapewa form utajaza na kubandika picha yako, then ukiirudisha hiyo form iliyokamilika utapigiwa mahesabu ya kodi yako kwa mwaka ambayo haizidi 100,000 TZS kwa mwaka endapo utakua umeomba TIN ya biashara.

Ukitaka kuepuka usumbufu wa kulipa hizi 100,000TZS kila mwaka wambie unataka TIN kwa ajili ya pikipiki hapo unaweza kulipa kama 30,000 TZS na hutalipia tena.
Ukipata TIN nenda mamlaka kama ya jiji au kama uko halmashauri, kutegemeana na wewe ulipo, huko utaenda kuomba leseni ya biashara na utalipia leseni hiyo, malipo haya hua ni mara moja tu, utaweza kusave sana kama utaipata leseni yako kutoka halmashauri na sio jiji wala manispaa kwa sababu halmashauri ni bei ndogo kiasi flani kuliko kwingineko.

Ukikamilisha hizo documents mbili zibebe pamoja na kitambulisho chako nenda kwenye office za mtandao husika wao watakuandalia hizo laini.
Faida ya njia hii: hizo laini ni mali yako hata zikipotea hutapata ugumu wa kurenew.

Hasara: mzunguko wa kuzipata ni mrefu kidogo, so inataka moyo.
 
Asante sana,kwa maelezo yako na kwa upande wa max malipo ni hivyo hivyo.
 
Yap ninayo TIN nilipewa wakati napata driving licence
 
Yap ninayo TIN nilipewa wakati napata driving licence

Ok fuata hatua nyingine sasa kuelekea mamlaka za jiji au halmashauri au manispaa ili upate leseni ya biashara.
Issue ya max malipo sina experience nayo jaribu kuulizia
 
Asante kwa mawazo yako.gharama kwa line zipo vipi
 
Samahan mkuu hata mm nna tin nmeipata kwny kuchukua driving licence na nipo dar maeneo ya airpot huko halmashaur ndo sehemu gani?
 
Nngeomba namba yako ya simu kwa msaada zaid
 

Habar. Mi nataka kuuliza je kama nmepata leseni ya biashara na tin no. Na nikaanza kufatilia till ya mpesa na haijatoka ni mwez wa pili. Vp naweza kwenda TRA ili waifunge iyo tin no. Ili ihesabike kama haifanyi kaz. Maana baada ya miez 3 inabidi kulipia tena kodi ilobaki, na sijaanza kufanya kazi wao wanataka kodi yao. Nisaidie wadau kwa ilo
 
Peleka taarifa TRA wambie hujapata till wasikilize watasemaje.
Kingine vodacom wanachelewesha till sana. Jitahidi kufuatilia mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…