Msaada: Kijana wa pikipiki yangu kafungua kesi akidai ni mali yake

Msaada: Kijana wa pikipiki yangu kafungua kesi akidai ni mali yake

kiria babu

Member
Joined
Sep 13, 2017
Posts
12
Reaction score
8
Nilimpa kijana pikipiki yangu awe anafanyia kazi ya bodaboda ile siku namkabidhi pikipiki ile usiku wake nikapata ajali hivyo ndugu yangu alipoteza maisha katika ajali hiyo wakati nikiwa ICU, kijana niliyempa pikipiki ile alipiga simu akaongea na ndugu yangu akidai ameibiwa pikipiki na hapohapo yupo namdhamini aliyemwaminisha awape pikipiki mabwana wale wakaamishe kitanda hivyo akawapeleka kituoni polisi na kuwafungulia mashitaka ya wizi wa kuaminiwa wakalala police asubuhi yake walipewa dhamana.

Nilipopona nikaenda kituoni pale kuwaeleza nikaambiwa kesi ishafunguliwa hivyo hatufungui kesi mbili nikamuuliza mimi ni mwenye mali na nina vigezo vyote kadi nk... hivyo aliyefungua kesi ile ni mtuhumiwa kwangu hivyo hastaili kufungua kesi bali anatakiwa anipe ushirikiano na wenzake wa kupata mali yangu.

Yaani mpaka sasa sijamuelewa mpelelezi wa kesi ile aseee maana nikiiitaji mrejesho hanipi wala hataki kuulizwa chochote. Nishauri wenzangu.
 
mhhh pole
kuna dili nahisi linachezwa..
kijana,mdhamini,polisi

kama inawezekana kufungua malalmiko kituo kingine..nenda
pambana hadi mali yako ipatikane.
 
Pole sana kaka,ila haki yako utaipata kama cyo hapa duniani bac akhera utaikuta haki yako
 
Occid nilimweleza na nikataka kubadili mpelelezi lakini alinijibu niende atanipigia cm nikaenda kufanya upelelezi mpaka ni nikajua pikipiki ile imeuzwa wapi matokeo yake mpelelezi alimtaka mtoa taarifa nikampeleka akaojiwa akawaeleza kilakitu lakini hakutaka kupeleka police sehemu hiyo bali anawaelekeza tuu matokeo mara mpelelezi akampeleka kwa occid ili waongozane lakini occid alisema kuwa kuna sehemu nyingine anakwenda hivyo awekwe lokap kwanza atamhuji usiku atimaye naenda asubuhi kufuata mrejesho naambiwa nije kesho mara tena naenda napata taarifa kuwa amewekewa dhamana na ndugu yake ambaye anafanya kazi tanesco hivyo atakuwa akiripoti ndipo nilipo mpaka sasa
 
Kama upo dsm we jitahidi tu uonane na RC makonda ni mtu smart sana anasaidia watu saana tatizo lako litatatuliwa
wangapi wenye matatizo wanaweza mfikia na asipokuwepo inakuwaje?
 
Pole sana mkuu...Tafuta mwanasheria akusaidie kwenye kesi yako hapo naona unachezewa mchezo mchana kweupe
 
Panda ngazi kwa ngazi, anza kwa ICD ikigoma kamuone mkuu wa wilaya utapata haki yako usijali. askari huwa wanashida sana sio kila hongo ni ya kuchukua.

Polee
 
Aaaghh mbona rahisi Sana hio kitu? Achana nao nenda Kwa Wakubwa zao, faster watakua wadogo Kama mbegu ya haradali
 
Ungewataja tu hapa boss wao yuko Jf na kapata PhD yake soon atamalizana nao
 
Back
Top Bottom