Ndugu yangu Anheuser, nikupongeze kwa changamoto uliyonipa,lkn iko hivi:
Sheria za kiislam hauwezi kuziita ni sheria za nchi bali zenyewe zinabaki kuwa sheria za dini ya kiislam, isipokuwa zinatambuliwa na mamlaka.
nikuulize kidogo, zipo sheria za nchi ya kenya, TZ,A.Kusin wanazo zao, marekani, Russia nk. sasa sheria za kiislam ni za nchi ipi?
kama kila nchi ina bunge linalotunga sheria za nchi hiyo, je ni bunge lipi hutunga sheria za kiislam?
katka nchi kuna mamlaka inayotunga sheria (bunge) na kuzifanyia marekebisho kuendana na matakwa ya nchi ndiyo maana sheria hizo huwa za nchi hiyo.
sheria za kiislam zinatokana na qur'an hivyo haziwezi kumilikiwa na nchi fulan bali humilikiwa na dini inayoamini kitabu hicho.
umeshawahi sikia bunge la TZ au nch yeyote inatunga au kufanya amendment sheria za dini?
hivyo basi kutambuliwa kwa sheria hiz hakuzifanyi kuwa sheria za nchi bali ni kwa jamii fulani au waumin wao.
pitia JALA s.11 uone applicability ya customary & islamic laws.