Msaada: Kiwanda cha kutengeneza toothpick Tanzania

Kama unataka kutafuta pesa usianze kuogopa mambo ya wakuu kutaka pesa kwanza. Hii Tanzania wanakuja wahindi, waarabu, wazungu hawajui hata Kiswahili, wanaelewana na hao wakubwa we unashindwa nini kuelewana nao uanzishe hiyo biashara yako??? Da production ya Toothpicks mtaji mkubwa kidogo, kwaiyo lazima ujipange... Machine wachina, wahindi hata sourth Africa unaweza pata, sema sourth gharama sana.
 
Ni wazo zuri, linataka thorough survey. one big challenge ni Mtaji. unatakiwa uwe na takriban 50M. kuhusu kibali sijajua vinatolewa kwa utaratibu gani, ila pia kama utaanzisha kama mjasiriamali mdogo unaweza kupata ahueni. pia naomba kupata mawasiliano ya LAT anaweza kunipa challenges alizokutana nazo.
 

Mtwange Pm, yumo humu.
 


Usiogope,50M inapatikana it only needs a smart and well adressed proposal..ujue challenges na jinsi ya kuzitatua,masoko lengwa both jumla na reja reja...ukiwa na mawazo na utayari amini hili linawezekana

Caution; Kuna watu wana pesa hawana mawazo so kuibiwa wazo au kudhulumiwa pia yamo.,sio kwetu tu hata kwenu yaaaapooo!!!!!!
 
Nshafatilia online kuhusu mashine za kutengeneza toothpick zipo hata za kuoperate mtu mmoja, yani hauhitaji kuwa na warehouse kuubwa kwajili Ya kufungua kiwanda, unaweza hata kufanyia kazi at your backyard, challenge niliyoiona ni jinsi Ya kupata raw materials(miti ambayo haina madhara na haina ladha chungu mdomoni), packaging materials na marketing. Na mashine nyingi nlizoziona ktk kugoogle kwangu ni za chini Ya $15,000
 
Patamu hapa. Ntakutafuta mambo yangu yakikaa fresh
 

Nilisha waza hii idea,nikafuatilia youtube jinsi machine zinavyo fanya kazi na Bei zake nikacheki Alibaba

Bei Si kubwa sana na changamoto ambazo nilikuja kuziona Ni kama hizo ulizo taja.

Kuhusu packaging Unaweza Kuanza na packaging nyepesi ya bei nafuu kama kutumia karatasi ngumu Au magome ya miti hiyohiyo inayokatwa kama malighafi. Au unaweza kufanya outsource ya packaging,kuna viwanda vya plastic bongo vinaweza kufanya hii kitu

Ila mimi nilifikiria kitu kimoja,hivi VETA Au SIDO hawawezi kutengeneza hizi machine ili upate kwa bei ya chini zaidi?
 

Recommended raw material ya tooth picks na skewers (vijiti vya mishikaki) ni Bamboo (mianzi Miti ambayo IPO kwa wingi mno katika mikoa ya nyanda za juu kusini mikoa kama iringa na mbeya botanical spicie za bamboo ambazo ni ngumu na pia unaweza kutengenezea ice cream sticks ni Arundaria Alpina

Nimewahi kufanya research undergraduate na pia ninayo business plan ya bishara ya utengenezaji wa mishikaki sticks (skewers) kwa kutumia mianzi miti
 

Hiyo plan yako ina jumuisha gharama za ununuzi wa machine? na umefanya cost benefit analysis ya machine za ukubwa tofauti?

Naipataje hiyo business plan?
 
Hiyo plan yako ina jumuisha gharama za ununuzi wa machine? na umefanya cost benefit analysis ya machine za ukubwa tofauti?

Naipataje hiyo business plan?

for sure .... financial plan is inclusive on the BP ... profit and loss account .... IRR and Return on investment

as well payback period

Process line ya kutengeneza toothpicks au vijiti vya mishikaki inajumuisha aina ya machine nane 8 .... very simple mashines .... ni vimashine kama zile za kukereza miguu ya stuli

Karibu
 
Wakuu Mbona naona kama BAMBOO na PALM trees zinafaa kwa kutengeneza TOOTH PICK,
na kama ni kwa uwakika hilo nadhani kuna haja ya kupeleka kiwanda KIGOMA.

mkuu ..... sahihi ni mkoa wa Mbeya ndiyo wenye potential ya Bamboo .... spicie iliyopo ambayo ndiyo ngumu na inafaa inaitwa 'Arundaria Alpina'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…