Msaada kuhusu Bidhaa kutoka kwenye mtandao wa Alibaba

Avictown

Member
Joined
Jan 16, 2018
Posts
98
Reaction score
56
Naomba msaada wenu, kuna bidhaa nimeiona Alibaba nikaipenda, muuzaji anasema yuko USA, tumebargain bei na kukubaliana. Tatizo nasita kumtumia hela make naogopa kutapeliwa. Naomba uzoefu kwa yeyote aliyewahi kuagiza bidhaa kutoka kwenye huu mtandao na ikafika Tanzania.
 

Kama hela unatuma kwenye akaunti ya Alibaba fresh,kama ni akaunti binafsi shtuka uwezekano wa kutapeliwa ni mkubwa
 
Kama hela unatuma kwenye akaunti ya Alibaba fresh,kama ni akaunti binafsi shtuka uwezekano wa kutapeliwa ni mkubwa
Akaunti ni ya mtu binafsi. Na ameweka Tangazo kwenye Alibaba. Nimeangalia nikaona kama vile alibaba hawauzi bidhaa bali wanakutanisha wateja na wauzaji. Naomba uzoefu wako mkuu kama ulishanunua hapo.
 
Akaunti ni ya mtu binafsi. Na ameweka Tangazo kwenye Alibaba. Nimeangalia nikaona kama vile alibaba hawauzi bidhaa bali wanakutanisha wateja na wauzaji. Naomba uzoefu wako mkuu kama ulishanunua hapo.

Mi uzoefu nina Aliexpress mkuu,kampuni ya mtoto wa Alibaba,huko unalipia kwenye akaunti ya kampuni,jaribu kwenda huko,kama ukiikuta hiyo product nunua huko kwani wapo poa tu na mzigo unafika ontime
 
Mi uzoefu nina Aliexpress mkuu,kampuni ya mtoto wa Alibaba,huko unalipia kwenye akaunti ya kampuni,jaribu kwenda huko,kama ukiikuta hiyo product nunua huko kwani wapo poa tu na mzigo unafika ontime
Asante sana mkuu.
 
Kuwa makini mzeee tena hao USA noma

Mimk nilitaka kununu atv ila bei ndo ilitisha tv ya 1.5 huku kule laki tatu kumpelelez vizuri mixer google nikakuta ni matapeli nikachukua ile screenshot ya utapeli nikawatumia nikamalizia na go f**k yourself
 
Asa
Kuwa makini mzeee tena hao USA noma

Mimk nilitaka kununu atv ila bei ndo ilitisha tv ya 1.5 huku kule laki tatu kumpelelez vizuri mixer google nikakuta ni matapeli nikachukua ile screenshot ya utapeli nikawatumia nikamalizia na go f**k yourself
Asante sana mkuu kwa alert yako muhimu sana.
 
Bado sijakata kiu juu ya hili,nataka kuagiza bidhaa fulani kutoka Alibaba,ila sijajua kama nitalipa baada ya kupata mzigo au kabla,sijajua nitaupokelea wapi mzigo wangu,msaada kwa hilo tafadhali.
 
Usije fanya malipo nje ya utaratibu uliowekwa kwenye website ya alibaba/aliexpress, bidhaa ndogo ndogo unazichukulia posta ila bidhaa kubwa wanawatumia DHL na wanakuletea ulipo
 
Na pia kwa utaratibu walioweka kwenye mtandao hakuna options ya kubargain, huyo uliyebargain naye ni tapeli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…