Habari wana jamvi, naomba msaada kuhusu Fao la uzazi kwa akina mama.
Mimi mke wangu amejiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSPF, mfuko huu umekuwa na utaratibu wa kutoa Fao la uzazi kwa wanachama wake wa kike pindi wanapojifungua na kukidhi vigezo vya Fao la uzazi vilivyowekwa.
Mapema mwezi huu mke wangu alifanikiwa kujifungua, na kwa kutambua kuwa anakidhi vigezo vya kupata Fao hili, niliamua kwenda Ofisi za PSPF Mwanza kwa ajili ya kumchukulia fomu ya maombi ya Fao la uzazi. Mara baada ya kufika ofisi husika majibu niliyopewa ndiyo yamenifanya nije hapa kuulizia.
Nilijibiwa kuwa PSPF wamepokea maelekezo/ waraka kutoka kwa Director General wao kuwa kuanzia sasa(since August 1) wamesitisha kutoa fomu za madai ya Fao hilo hadi pale maelekezo mengine yatakapotolewa.
Ikumbukwe kuwa ombi la Fao hili hudaiwa ndani ya miezi mitatu tangu kwa mdai kujifungua, nilijaribu kuwaomba wanipe uthibitisho wa kwamba nilifika ofisini kwao kuchukua fomu hizi lakini sikufanikiwa kwa sababu ya maelekezo kutoka kwa DG wao, hili nalo nilikataliwa.
Kwa ufahamu wangu (naweza kurekebishwa) Fao la uzazi bado linatambuliwa hata kwa sheria mpya ya mifuko ya hifadhi ya jamii ( Baada ya kuunganishwa), sasa ni kwanini wametoa maelekezo haya bila hata kujulisha umma wa Mtanzania na bila hata ya kutoa mbadala wa nini wadai hawa wafanye ili kuja kupata haki yao hata hapo baadaye?
Kufuatia hali hii wadau mnatoa ushauri gani? Au kuna mwenye uelewa mwingine juu ya hili?
Mimi mke wangu amejiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSPF, mfuko huu umekuwa na utaratibu wa kutoa Fao la uzazi kwa wanachama wake wa kike pindi wanapojifungua na kukidhi vigezo vya Fao la uzazi vilivyowekwa.
Mapema mwezi huu mke wangu alifanikiwa kujifungua, na kwa kutambua kuwa anakidhi vigezo vya kupata Fao hili, niliamua kwenda Ofisi za PSPF Mwanza kwa ajili ya kumchukulia fomu ya maombi ya Fao la uzazi. Mara baada ya kufika ofisi husika majibu niliyopewa ndiyo yamenifanya nije hapa kuulizia.
Nilijibiwa kuwa PSPF wamepokea maelekezo/ waraka kutoka kwa Director General wao kuwa kuanzia sasa(since August 1) wamesitisha kutoa fomu za madai ya Fao hilo hadi pale maelekezo mengine yatakapotolewa.
Ikumbukwe kuwa ombi la Fao hili hudaiwa ndani ya miezi mitatu tangu kwa mdai kujifungua, nilijaribu kuwaomba wanipe uthibitisho wa kwamba nilifika ofisini kwao kuchukua fomu hizi lakini sikufanikiwa kwa sababu ya maelekezo kutoka kwa DG wao, hili nalo nilikataliwa.
Kwa ufahamu wangu (naweza kurekebishwa) Fao la uzazi bado linatambuliwa hata kwa sheria mpya ya mifuko ya hifadhi ya jamii ( Baada ya kuunganishwa), sasa ni kwanini wametoa maelekezo haya bila hata kujulisha umma wa Mtanzania na bila hata ya kutoa mbadala wa nini wadai hawa wafanye ili kuja kupata haki yao hata hapo baadaye?
Kufuatia hali hii wadau mnatoa ushauri gani? Au kuna mwenye uelewa mwingine juu ya hili?