Hivi karibuni niliagiza bidhaa kutoka nje ya nchi,nashukuru imefika salama,nimepewa gharama za kodi za mashine husika na cost za delivery order. Kulichonistua ni hapa kwenye gharama za delivery order, wakala anahitaji zaidi ya dola 250,kwakweli hili limenistua sana maana hiko kiasi kinazid hata cost za CIF,sina uzoefu na haya mambo ila naamini iki kiasi kimekuzwa sana,naombeni ushauri wenu,ni kwa namna gani naweza kupata gharama halisi za D.O
Nashukuru sana mkuu kwa mawazo yako,angalau yamenipa mwanga wa wapi pa kuanziaDerivery Order (DO) utolewa na shipping Lines/Agents.
Wakati mwingine mtu unayekutana naye pale Shipping Line/agent anataka akupige kama wewe ni mgeni wa mambo hayo. Kabla hujalipia DO kwenye carrier agent wako, fanya utafiti mdogo kwenye shipping line zingine. Jifanye unataka kuagiza mzigo nje na ungependa utumie kampuni yao. Hivyo omba quatation ya gharama. Ukiondo freight. Wambie wakupe hata port charges. SUMATRA wanatoa Tarrif za Freight, sina uhakika kama wanatoa tarrif za D/O pia. Ukiwa na nafasi tembelea website ya SUMATRA kujirithisha. Ila kama nilivyoshauri fanya hako kautafiti. Otherwise omba kuonana na GM wa kampuni husika. Usijekuwa umepigwa na watu wa Sales ambao ndo wanahusika na hizo DO