Msaada, kuhusu kuahirisha mwaka

Msaada, kuhusu kuahirisha mwaka

Kivule

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2012
Posts
639
Reaction score
662
Habarini ndugu, poleni na majukumu ya kila siku. Mimi nilikua naomba mnifahamishe vitu ambavyo mwanafunzi anatakiwa avifanye endapo amechaguliwa chuo fulani na amepata mkopo lakini hataki kusoma iyo kozi ivo anataka afanye application upya mwakani, je afanyaje ili akiapply mwakani asije akaathiri kupata mkopo upya mwakani kama ana vigezo??? ahsanteni.
 
utaritibu wa kuahirisha mwaka lazma uende chuo ulichopangiwa usajiliwe kwanza then ndo watakupa hatua za kufuata ikiwemo kuandika baru ya kuahirisha. hakikisha unafanya hvo coz hela itaendelea kwenda chuo na wajanja wanaweza kuifanyia mambo
 
Fanya registration kwanza chuo husika then ndo ufate taratibu za chuo jinsi ya kupostpone.!!
 
Habarini ndugu, poleni na majukumu ya kila siku. Mimi nilikua naomba mnifahamishe vitu ambavyo mwanafunzi anatakiwa avifanye endapo amechaguliwa chuo fulani na amepata mkopo lakini hataki kusoma iyo kozi ivo anataka afanye application upya mwakani, je afanyaje ili akiapply mwakani asije akaathiri kupata mkopo upya mwakani kama ana vigezo??? ahsanteni.

Nimevyokuelewa ni kwamba, hutaki kusoma kozi uliopangiwa. Kama ni hivyo na katika chuo ulichopangiwa kuna kozi unayoipenda, ni vyema ukaenda kuripoti kisha ukafanya mchakato wa kubadili kozi. 'Muda ni mali'
Kama unampango wa kufanya upya 'application' mwakani, ina maana unaweza kuchaguliwa chuo kingine; hapa haina haja ya kufika chuoni ulipopangiwa mwanzo na kufanya usajili. Kufanya usajili ili uahirishe mwaka, ni pale tu utapokua na lengo la kurudi chuo hapo mwakani. Fahamu usajili huhitaji pesa.
Chakufanya wewe nenda bodi ya mikopo ukatoe taarifa ya kusitisha mkopo wako. Hii ni muhimu kwani hukuhakikishia uhakakika wa kupata mkopo mara wanapoomba kwa mara nyingine. Ukiacha kufanya hivyo, mkopo wako utaliwa na itakubidi kulipa 25% ya pesa iliyoliwa mara utapohitaji kupewa mkopo kwa mara nyingine.
 
Ahsante sana kaka kwa ushauri wako mzuri kabisa, nilichofanya ad sasa nimejisajili ndio ilihitaji hela lakini mkopo nilipata mkubwa km 90% ivyo baada ya kujisajili wiki iliyopita niukaandika barua ya kuhama kozi na majibu yanatoka baada ya wiki 2 apo UDSM. Sasa nimeamua nisipofanikiwa kubadili kozi ndo niache chuo nifanye application upya mwakani na niandike barua loan board km ulivoshauri, ahsante.
 
Ahsante sana kaka kwa ushauri wako mzuri kabisa, nilichofanya ad sasa nimejisajili ndio ilihitaji hela lakini mkopo nilipata mkubwa km 90% ivyo baada ya kujisajili wiki iliyopita niukaandika barua ya kuhama kozi na majibu yanatoka baada ya wiki 2 apo UDSM. Sasa nimeamua nisipofanikiwa kubadili kozi ndo niache chuo nifanye application upya mwakani na niandike barua loan board km ulivoshauri, ahsante.


Mkuu ufikirie vizuri uamuzi wako wa kuahirisha mwaka,mwakani ushindani wa kozi zinazodhaniwa ni nzuri utadouble,

Nina marafiki zangu wawili imewacost sana hiyo kitu

Just to remind,if u are sure..move on
 
Ahsante kwa ushauri wako mzuri kabisa ila ngoja nifanye nachoamini.
 
kwani uliomba kozi gani na wamekuchagulia kozi?,ni bora uangalie kozi inamarket hata kama upendi ww komaa tu remember time does not backup think twice
 
Back
Top Bottom