Msaada kuhusu mikopo ya wafanyakazi CRDB

mutu murefu

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2017
Posts
996
Reaction score
2,636
Habari za Asubuhi wanajamvi,

Nina imani kuna wafanyakazi wenye ufahamu na jambo hili,

Naombeni msaada wenu,

Nataka kujua ni kiasi gani cha juu kabisa cha mkopo ambacho mfanyakazi anaweza kukopa CRDB na kwa limit ya miaka mingapi. Mfano kama mshahara ni 980,000. Je inawezekana kuchukua mkopo limit kiasi gani na kwa makato ya shilingi ngapi kwa mwezi na kwa miaka mingapi.

Naomba mawazo na kujenga.

Nawasilisha
 
Hawatoi tena mikopo mkuu
Wanatoa kwa baadhi ya branches, baadhi wanafanya loan recovery kwanza nadhani ni baada ya athari za watumishi hewa. hata hivyo watafanya loan recovery kwa kipindi fulani then braches zote zitaendelea kutoa loan kama kawaida.

Hakuna bank itaweza ku-exist pasopo kukopesha maana deposits haziwezi ku accomodate Bank ku- exist kwa kiasi ambacho kinatakiwa.
 
Hiyo Tzs.980,000 ni basic au take home?
 
Naamini take home yako haitazidi 750000 kwa makadirio ya juu.

Kwa kubashiri tu, unaweza kukopa kuanzia milioni 12 hadi 15 kutegemea na tawi si unajua hawa jamaa huwa wengine wanaamua kufumba macho though wakifuata sheria 13 haizidi.

Ni mawazo yangu tu, sina elimu ya ukokotoaji wala nini, unaweza kuniamini au kunipuuza.
 
Hua kuna Objective ways ya ku calculate mkuu kikubwa isizid kiwango kilichowekwa na sheria ya nchi ya ukopaji ya 1/3ya Gross Salary
 
Yeah, naamini sasa branches nyingi zimeanza kutoa
 
Reactions: SDG
Sasa hivi wameanza Kutoa mikopo, nenda kwenye tawi la crdb lililo karibu yako na salary slip utapata jibu zuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…