Leo katika pitapita zangu nikaona tangazo la NMB kuwa kwa sasa wanatoa mkopo nafuu kwa watumishi na wamesema ni asilimia 11% pia kuzingatia 1/3 ya
mshahara.....
Maswali yangu..
1. Iyo 1/3 ya mshahara inahesabikaje? Je, ni katika basic salary au take home?
2. Mfano mtu anaepokea take home ya tsh 470'000/= baada ya makato kutoka bodi huyu 1/3 yake ni shiling ngapi??
3. Mwenye uelewa hapo hiyo riba ya 11% kwa mwaka mfano mtu uchukue milioni 10, utarejesha shilling ngapi baada ya miaka 5?
Naomba kuwasilishaaa