Penny hongera sana kwa kuwa mama mtarajiwa, Hiyo ni hatua muhimu sana kwenye maisha yako na ni vizuri kwa kuwa inaonesha umejiandaa kimwili na kiakili. Ni vizuri pia kama mwenzi wako pia akawa karibu na wewe kipindi hiki muhimu cha maisha yenu kama wazazi watarajiwa.
Kwa kawaida kipindi cha ujauzito kimegawanywa katika makundi matatu ya takriban miezi mitatu kila kundi. Miezi mitatu ya kwanza ni kipindi muhimu kuliko vyote kwa sababu ndo viungo vya mtoto vinaundwa na vipindi vingine ni ukuaji wa kawaida. Utumiaji wa dawa na vyakula vyenye kemikali ambazo zinaathiri mgawanyiko wa chembechembe za mwili ( cell division) haitakiwi kabisa kwa sababu zaweza kuharibu maumbile ya kiumbe au hata kuharibu mimba. Ni vizuri kupata maelekezo ya daktari kabla ya kutumia aina yoyote ya dawa.
Kwa upande wa vyakula ni vizuri kutumia chakula bora ( balanced diet) ni muhimu kwa ukuajia wa mtoto na kwa afya yako pia.
Vyakula vinavyoongeza damu ni muhimu sana matunda na mboga za majani, ni muhimu pia kunywa maji kwa wingi.
Ukifikisha miezi mitano ya ujauzito anza clinic ya wajawazito kwenye hospitali au kituo karibu nawe.
mambo muhimu ya kuzingatia:
Damu au maji kutoka ukeni
mtoto kupunguza kucheza
maumivu makali ya tumbo
Homa
Kuvimba miguu
Kuongezeka uzito kwa kasi sana ( > 5kg per month)
etc..........
Uwaone wataalamu mapema.
Otherwise kwa niaba ya wana JF nakutakia miezi tisa yenye utulivu na kila la kheri kwa kipindi chote cha ujauzito wako.
regards
Penny hongera sana. uashauri aliokupa M/Jadi ni mzuri na cha kuongezea ule samaki kwa wingi na usifanye kazi nzito
Hongera sana Penny, ushauri wa mzee wa jadi ni sahihi kabisa! ila nataka kuongezea jambo kidogo maana namimi nimemaliza ngwe hii miezi sita iliyopita. Kuhusu kuhudhuria kriniki, siku hizi kama huna tatizo lolote wanashauri uhudhurie kriniki mara nne au tano tu. Inashauriwa katika kila kundi kama alivyotanabaisha Mganga wa jadi angalu mara moja. kwahiyo nashauri angalau uanze Kriniki miezi mitatu (Kundi la kwanza) baada ya hapo daktari ndo atakwambia urudi lini, kufuatana na utakavyoamabiwa. Lakini pia chagua kriniki nzuri sio ili mradi kriniki. Na pia angalia hakikisha kila kipimo kilichooneshwa katika kadi ya kriniki unakifuatilia na kujua kinamaanisha nini. Wakati mwingine nesi anaweza akakupima BP akairekodi bila kukuambia kama iko juu, chini au kawaida na vipimo vingine kama mkojo, kiasi cha damu nk ni muhimu kupima katika kila hudhurio la kriniki. Nakutakia kila laheri Mungu akulinde wewe na mtoto ili mwisho wa yote tabasamu lako lizidi hilo ulilonalo sasa.Penny hongera sana kwa kuwa mama mtarajiwa, Hiyo ni hatua muhimu sana kwenye maisha yako na ni vizuri kwa kuwa inaonesha umejiandaa kimwili na kiakili. Ni vizuri pia kama mwenzi wako pia akawa karibu na wewe kipindi hiki muhimu cha maisha yenu kama wazazi watarajiwa.
Kwa kawaida kipindi cha ujauzito kimegawanywa katika makundi matatu ya takriban miezi mitatu kila kundi. Miezi mitatu ya kwanza ni kipindi muhimu kuliko vyote kwa sababu ndo viungo vya mtoto vinaundwa na vipindi vingine ni ukuaji wa kawaida. Utumiaji wa dawa na vyakula vyenye kemikali ambazo zinaathiri mgawanyiko wa chembechembe za mwili ( cell division) haitakiwi kabisa kwa sababu zaweza kuharibu maumbile ya kiumbe au hata kuharibu mimba. Ni vizuri kupata maelekezo ya daktari kabla ya kutumia aina yoyote ya dawa.
Kwa upande wa vyakula ni vizuri kutumia chakula bora ( balanced diet) ni muhimu kwa ukuajia wa mtoto na kwa afya yako pia.
Vyakula vinavyoongeza damu ni muhimu sana matunda na mboga za majani, ni muhimu pia kunywa maji kwa wingi.
Ukifikisha miezi mitano ya ujauzito anza clinic ya wajawazito kwenye hospitali au kituo karibu nawe.
mambo muhimu ya kuzingatia:
Damu au maji kutoka ukeni
mtoto kupunguza kucheza
maumivu makali ya tumbo
Homa
Kuvimba miguu
Kuongezeka uzito kwa kasi sana ( > 5kg per month)
etc..........
Uwaone wataalamu mapema.
Otherwise kwa niaba ya wana JF nakutakia miezi tisa yenye utulivu na kila la kheri kwa kipindi chote cha ujauzito wako.
regards
KWANZA-Penny hongera sana dada Mungu akupiganie vya kutosha ktk kipindi chote cha ujauzito wako Siha njema akujaalie na Shari akuepushie.
PILI-Mganga wa Jadi vyakula vya kuongeza damu nivip namboa na mifano plz[/I][/I][/I].
Kuna kitu naona kimesahaulika:
Penny unatakiwa as much as possible uwe na mawazo mazuri kila mara, acha kukasirika ovyo na kisirani pale inapowezekana kama mimba haikusumbui. Kuna vijitabia vya watoto tunakuwa tumewapatia sis wenyewe katika process ya kubeba mimba.Uwe na raha na pia kumsemesha mwano aliye tumboni - hasa mweleze mnavyompenda n akumtarajia!
Sijui mwenzio mliyoshirikiana katika uumbaji naye anashiriki vipi katika safari yako kubeba tumbo miezi tisa.Na yeye mpe nafasi - ashike tumbo lako, asikilize mateke pale mtoto atakavyoanza kucheza tumboni, akusindikize clinic, mpe card yako ya clinic asome na mweleweshe kinachoendelea.
Kuzaa kwa mwanaume siyo kupanda mbegu tu, afuatilie hadi mazao yanapotokea.
Good luck and enjoy the process of motherhood.
Kutofanya kazi nzito inategemeana na tabia za mimba.
Reolaston.Kila mama mjamzito huwa anabehave tofauti kuna mwingine kuanzia day one mpaka mwisho ni mchapa kazi hivyo inategemeana na aina ya kazi uisemayo kama ni ya kutumia akili sana au uzito wa ukubwa (kgs tani)
Mke wangu kuanzia day one mpaka mwisho alikuwa akifanya kazi na hakupa bed rest hata moja na wala hajawahi kutapika na uchungu umeaupatia kazini hivyo inategemana kwakweli siyo uniform kwa kila mtu.
Nawasilisha.