Ze Heby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2011
- 5,636
- 6,178
Wakuu wangu,siku 3 zilizopita nilipatwa na ajali ya kuumwa na nyoka au mdudu mguuni(jirani na kisigino) nilipokuwa nikitoka darasani kuelekea bwenini majira ya saa 7 usiku.Nasema nyoka au mdudu sababu sikumuona sababu ya taharuki na giza lililokuwepo ingawaje hakukuwa na jeraha wala meno ya nyoka.Tatizo nililo nalo ni kuwa nililetwa hospitali nikachomwa (hadi sasa) sindano nne za hydrocortisone sodium succinate lakini effect yake imekuwa taratibu sana kiasi kwamba sipati usingzi usiku kucha kwa maumivu.Pia nesi aliniambia kuwa sindano moja tu huwa inatosha kabisa kumaliza maumivu yote.Je,hii ni kawaida kwangu?Na pia naomba kusaidiwa njia mbadala ili nipone mapema niweze kurudi kwenye ujenzi wa taifa.Natanguliza shukrani wakuu wangu