Msaada kuhusu tetenus (Pepopunda)

mwibi

Senior Member
Joined
Jul 28, 2016
Posts
131
Reaction score
79
Wanajamvi leo unaulizia kuhusu tetanus ni nini na ukiumia umapaswa kuchoma sindano hiyo baada siku ngapi au haina muda wa kuchoma baada ya kuumia
 
Kwanza nenda hospital utapata majibu yakinifu
 
Wanajamvi leo unaulizia kuhusu tetanus ni nini na ukiumia umapaswa kuchoma sindano hiyo baada siku ngapi au haina muda wa kuchoma baada ya kuumia
Unataka uchome sindanio ya tetanus ndani ya masaa 48 ya kuumia. Usifanye masihara wale wadudu wakikuvamia huponi hata iweje. Wala hakuna mtishamba wa kukuponyesha.
 
Unataka uchome sindanio ya tetanus ndani ya masaa 48 ya kuumia. Usifanye masihara wale wadudu wakikuvamia huponi hata iweje. Wala hakuna mtishamba wa kukuponyesha.
Uwezekano wa kuishi 50/50 ukipata huduma nzuri ya ICU mapema. Wapo wanaoishi.
 
Uwezekano wa kuishi 50/50 ukipata huduma nzuri ya ICU mapema. Wapo wanaoishi.
Itakuwa ilikuwa bahati sana aliwahi kabla wadudu hawa ja attack nervous system yote. Yaani ugonjwa hatari huu.
 
Tetanus ni ugonjwa unaosababishwa na bacteria waitwao clostridium tetani. Huingia kwenye mwili mara nyingi kuoitia kwenye jeraha. Sindano ya anti tetanus unapaswa uchome mara tu baada ya kupata jeraha ili mradi isipite masaa 72. Ni vizuri ukachoma dozi nzima ili upate kinga ya maisha. Dozi ni sondano 5 ambazo huchomwa kwa ratiba maalum. Ukipata tetanus kama walivyosema wenzangu uwezekano wa kupona ni mdogo, wengi hufariki japo wapo wanaopona. Kumbuka kinga ni bora kuliko tiba.
 
Ila nimejikata kidogo kwenye kidole nimechoma sindano za PPF lakin uvimbe ukiendelea kukua so ndio nimechoma Leo hiyo sindano imeadimka kwenye mahospitali mengi ila nimechoma baada ya siku 10
 
Ila nimejikata kidogo kwenye kidole nimechoma sindano za PPF lakin uvimbe ukiendelea kukua so ndio nimechoma Leo hiyo sindano imeadimka kwenye mahospitali mengi ila nimechoma baada ya siku 10
Hapo hautapata kinga kwa jeraha hili, ila sio vibaya kuendelea na dozi ili upate kinga kwa majeraha yajayo. Kumbuka kuwa sindano ya kwanza haina kinga mpaka utakapo choma ta pili baada ya wiki 4, ndio utapata kinga ya miaka 3.
 
Hapo hautapata kinga kwa jeraha hili, ila sio vibaya kuendelea na dozi ili upate kinga kwa majeraha yajayo. Kumbuka kuwa sindano ya kwanza haina kinga mpaka utakapo choma ta pili baada ya wiki 4, ndio utapata kinga ya miaka 3.
Nilivyoenda pia wamenambia hivyo hivyo unavyosema
 
Kinga ya Tetanus ziko za aina mbili ya kwanza ni T.T iko kwenye form ya toxoid yaani sumu iliyopozwa ambayo ina act kama antigen kuusaidia mwili kutengeneza kinga zidi ya Ugonjwa wa Tetanus na ya pili ni ATS Anti tetanus Sera hii ni direct antibodies ambazo zinazuia vijidudu vya Tetanus Maamuzi ya kinga Ipi itolewe baada ya jeraha inategemea aina ya jeraha ,kisabaibishi cha hilo jeraha na dalili za tetanus ,wadudu wa tetanus wanapatikana kwenye jeraha chafu na Lililo deep(penetrated wounds ,Animal bite,human bite,wound resulted from rusty objects) na kinga kuu ya tetanus ni kusafisha jeraha kwa maji ya kutosha na sabuni,kutoa dead tissues na antibiotics na TT akapata hata baada ya 72 hrs bila madhala yeyote ,ila kama mgonjwa amekuja mfano ameraluliwa na mamba kidonda kimechukua muda kupata huduma na ameanza kuonyesha dalili ATS ndio mwake halafu TT inafuata.ili kupata kinga kamili ya tetanus inabidi mtu apate dozi 5 ktk kipindi cha mwaka ina maana ukiumia ukaanza TT ni vzr umalize dozi zote ili upate life long immunity sio kila unapoumia unachoma!ie hizo dozi ni sawa na zile mama mjamzito anachoma ili kumkinga mtoto na Neonatal tetanus ambayo source yake ni maambukizi kupitia kitovu ,kinga nyingine ya Tetanus ni DPT hii inamkinga mtoto kwa miaka 5 ya utoto!
 
Asante silasy umedadavua kwa undani sana
 
Nashukuru hili tatizo lilipata matibabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…