Msaada kuhusu upatikanaji wa mashamba ya kununa Morogoro

mbugabire

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2012
Posts
261
Reaction score
87
Wasalaam wakuu.
Niwape pole na majukumu ya kipindi hiki cha siku kuu.
Husika na kichwa cha habari hapo juu.
Ninahitaji kununua mashamba mkoa wa Morogoro kwa bei ndogo wa lengo la kuendeleza shughuli za kilimo.
Nitashukuru kwa ushirikiano wenu
 
Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.....unapendelea wilaya gani!Lakini pia malengo yako ni kutaka kulima mazao gani ili iwe rahisi kushauriwa!
 
Mkoa wa Morogoro ni mkubwa sana.....unapendelea wilaya gani!Lakini pia malengo yako ni kutaka kulima mazao gani ili iwe rahisi kushauriwa!
ningependa kupata katika wilaya yoyote, kuhusu mazao nitalima kulingana na kinachokubali zaidi katika eneo husika
 
Njoo wilaya ya mvomero, pande za kata ya mzumbe, sehem inaitwa lubungo, utapata mashamba hata laki 2 kwa eka,
Ukidevelop facilities km kisma na pump utalima any horticultural crop Km sweet corn, orange sweet potato, tomato any variety, sweet pepper, onion na vegetables zote za tropical na sub tropical, na utapga hela nzur kuliko hata mshara wako.
Karibu Morogoro.
 
-->anayefikiria kulima Moro anaakili sana maana ni rahisi kuyafikisha mazao dar...
*pia upon Uzi huku wa mashamba utafute mkuu.
 
asante sana mkuu, mchango wako unanitia moyo. Naomba kupata mawasiliano yako kama upo maeneo ya huko mvomero ili unisaidie kufanikisha ununuzi wa mashamba nianze kilimo mwakani rasmi.
 
-->anayefikiria kulima Moro anaakili sana maana ni rahisi kuyafikisha mazao dar...
*pia upon Uzi huku wa mashamba utafute mkuu.
-->anayefikiria kulima Moro anaakili sana maana ni rahisi kuyafikisha mazao dar...
*pia upon Uzi huku wa mashamba utafute mkuu.
asante sana mkuu, naomba link ya huo uzi nipate taarifa zaidi
 
Karibu ,kuna eka 50 zinauzwa mvomero nyuma ya ofisi za wilaya ya mvomero ni eneo zuri waweza lima tikiti, maharage mahindi miti nk 0783 656554
 

Vizuri ukamtaadhalisha pia na vurugu za wafugaji....huko Lubungo si ndiko aliuawa mkulima na wafugaji wa jamii ya kisamai mwaka huu???...Mpe mwenzio tahadhali zote akija ajue kabisa....kwa wilaya ya mvomero bora ungemshauri aende maeneo ya Kanga,Mziha au Kibati,ardhi ni nzuri na yenye rutuba lakini pia hakuna migogoro na wafugaji kama hapo Lubungo,Dakawa na maeneo ya karibu!
 
Hata m Nina mpango wa kutaka kununua hekari 10 hapo morogoro ,nimefikiria serikali ikiha100 DODOMA. Nitafanya kilimo hapo morogoro na. Kuuza mazao doodoma
 
nimeupata ushauti wako mkuu, naomba uniasaidie kuniunganisha na wenyeje wa maeneo ya huko ulipotaja ili nipate mashamba mazuri yasiyo na migogoro
 
nimeupata ushauti wako mkuu, naomba uniasaidie kuniunganisha na wenyeje wa maeneo ya huko ulipotaja ili nipate mashamba mazuri yasiyo na migogoro

Nitakutumia namba za simu za wenyeji wa huko mkuu,watakusaidia!Nina watu huko nafahamiana nao hivyo ondoa shaka!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…