Msaada kuhusu usimamizi wa mirathi.

Likwanda

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2011
Posts
3,922
Reaction score
1,149
Ndugu zangu naombeni msaada wa sheria inayohusu haki ya msimamizi wa mirathi baada ya mirathi kutoka.

Mama yangu alipata mtu ambaye alijitolea kua msimamizi wa mirathi, lakini baada ya Mirathi kutoka anadai kuwa kisheria Msimamizi wa mirathi inatakiwa apewe Thelusi moja ya thamani yote ya mirathi.

Je ni sahihi kisheria? Ni hayo tu ndugu zangu.
 
Fungua website ya RITA wanaweza kuwa wametoa ufafanuzi wa kutosha.
 
hakuna kitu kama hicho sheria za mirathi zinawatambua watoto,mke/wake/mume,baba na mama inategemeana na dini pamoja na mila za mlengwa lakini msimamizi wa mirathi kazi yake ni kugawa mirathi alivyoelekezwa kwa walengwa na hana fungu ktk mirathi na wala hakuna sheria ya namna hiyo isipokuwa kama yuko ktk kundi mojawapo ya niliyoyataja hapo juu.
 

Asante sana Mkuu, kwamsaada wako.
 
lakini baada ya Mirathi kutoka anadai kuwa kisheria Msimamizi wa mirathi inatakiwa apewe Thelusi moja ya thamani yote ya mirathi.

Je ni sahihi kisheria?

Kama mirathi ilishatoka ina maana beneficiaries walishalipwa cheki zao (maana siku hizi kila mtu anapewa chake), sasa hilo suala la theluthi moja (1/3) linatoka wapi?
 
Wakuu hata kidini, kimila nako ni "kisheria!" Mmesahau mambo ya Islamic Law, Customary Law, nk? Au neno "kisheria" lina maana gani kwenu?
Hapa mkuu, inamaana kuwa mirathi imefuata sheria ya Mirathi au sheria ya kidini. Kwa maana kama utafuata sheria ya Dini Inamaana kua itabidi kufuata utaratibu kama Dini inavyoelekeza na hata mgawanyo lazima ufanyike ktk taasisi maalum kwa mujibu wa imani, sasa kwa upande wangu mimi nilipenda kujua kupitia Sheria yenyewe ya mirathi, je kuna kipengele kinachotaja haki halisi ya Msimamizi wa mirathi ktk Mirathi aliyosimamia? Sifahamu sheria hivyo kama nimekosea unaweza kunielekeza zaidi.
 
View attachment 95787View attachment 95787
View attachment 95787 download cover hapa chini

View attachment 95787
View attachment 95787
 
Kama mirathi ilishatoka ina maana beneficiaries walishalipwa cheki zao (maana siku hizi kila mtu anapewa chake), sasa hilo suala la theluthi moja (1/3) linatoka wapi?

Sawa kabisa kama ulivyo eleza hapo juu, ila msimamizi wa Mirathi yeye sio beneficiar ktk hiyo mirathi. Je ni kweli anatakiwa alipwe na beneficiary hiyo thelusi aliyosema? ndilo swali langu.
 
Sawa kabisa kama ulivyo eleza hapo juu, ila msimamizi wa Mirathi yeye sio beneficiar ktk hiyo mirathi. Je ni kweli anatakiwa alipwe na beneficiary hiyo thelusi aliyosema? ndilo swali langu.

Kifupi: Hakuna Sheria inayoeleza kwamba Msimamizi wa Mirathi anatakiwa alipwe theluthi (1/3) ya mirathi hiyo.
Hata hivyo, kama kuna gharama alizotumia Msimamizi, km usafiri, mazishi, nk anatakiwa arudishiwe!
 
Masuala yote yanayohusu mali za marehemu baada ya kifo kama yalivyo majanga mengine ya kijamii nasimamiwa na Sheria za Tanzania,bila kujali dini, mila nk. Sheria ni lazima itasimama na kuwa chombo cha mwisho katika kutoa maamuzi..Msimamizi wa mirathi anaweza kuwa katika sehemu mbili either akiwa kama beneficiary au non beneficiary( mnufaika au asiye mnufaika wa mirathi) kama wengine walivyofafanua...lakini pia jukumu la msimamizi wa mirathi wa aina yeyote ni kuhakikisha kwamba anasimamia mgawanyo wa mali za marehemu kulingana na maelekezo na matakwa ya marehemu mwenyewe( kama upo wosia) au kufuatana na utaratibu wa sharia..na kama naye ni beneficiary naye sharia inamhusu katika kupata mgawanyo huo, lakini kama siyo mnufaika basi jukumu lake linaishia tu pale mgawanyiko utakapokuwa umekamilika.....hapewi kitu chochote.
 
Kifupi: Hakuna Sheria inayoeleza kwamba Msimamizi wa Mirathi anatakiwa alipwe theluthi (1/3) ya mirathi hiyo.
Hata hivyo, kama kuna gharama alizotumia Msimamizi, km usafiri, mazishi, nk anatakiwa arudishiwe!

Asante sana mkuu Buchanan, nimekeelewa vizuri sana. Kwa vile ghalama zote za ufuatiliaji nililipa mimi hakuna tena marejesho, hivyo nimemuandalia asante yake ambayo nimeona itamfaa.
 
Last edited by a moderator:

kisheria siyo sahihi, anachoruhusiwa tu kuchukua ni kufidia gharama zozote alizoingia katika kufanikisha kupata uteuzi wa mirathi na kugawa mirathi. sio zaidi ya hapo. Gharama hizo zinajumuisha fedha alizolipia kufungua akaunti zenu kama hamkuwa nazo, fedha alizotumia kama nauli za kufuatilia, kununua chakula, kulipia gharama za mahakama na zozote ambazo mtaridhika kuwa lazima angetumia ili kufanikisha suala lenu. cha kufanya mpelekeni mahakamani kwa hakimu aliyetoa uamuzi muelezeni anataka kuwadhulumu haki yenu kisha atawasaidia. tena muiombe mahakama ifute uteuzi wake wa usimamizi wa mirathi na badala yake ateuliwe mama yenu au yeyote kati ya watoto wa marehemu mwenye umri kuanzia miaka 18. mkiona vinginevyo muombe mahakama imlazimishe alete thamani ya mirathi mahakamani kisha muombe mahakama iwagawie kila mtu stahili yake na kufunga mirathi. hata hivyo ni vizuri ateuliwe mmoja wenu kuwa msimamizi wa mrithi kwani zinaweza kujitokeza mali zingine za kufuatilia na kugawana, huyo ndicho atakachokifanya

ukiwa na swali uliza tena
 
Asante sana Mh. assuredly4 maelezo yako pia nimeyaelewa vizuri sana. Kwakua gharama zote za kufuatilia pamoja na mahitaji yote muhimu pamoja na posho za kufuatilia tulilipa wenyewe, tupo ktk hatua za kumuondoa ktk usimamizi kabla B.O.T hawajatulipa hili kuepuka visasi na migogoro isiyo na sababu si unajua tena wengine huwa wanawaza kudhulumu tu.
 
Last edited by a moderator:

nawatakia kila la kheri, Mungu awasaidie na kuwatangulia katika kila hatua
 
Ndio maana tunataka mahakama ya Kadhi,kwa muislamu hili wala halikua hata na mjadala kama mahakama ya kadhi ikiwepo.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…