Mchumba wangu anasumbuliwa na tatizo la kuwashwa sehemu za siri na maumivu makali wakati wa kujamiana.
Naombeni msaada wa kitaalamu.
Atakuwa anayo maradhi ya Mzio (allergy) au Fungus sehemu zake za siri anitafute nipate kumtibia ili aweze kupona.
MUWASHO SEHEMU ZA SIRI BAADA YA TENDO
HUSABABISHWA NA NINI
Kujamiana ni kitendo cha heshima katika maisha ya ndoa ya binadamu. Ni tendo linalohusiana na uumbaji na kwa sababu wote tuliumbwa ni vyema tukaliheshimu kama tunavyojiheshimu wenyewe.
Kuna sababu kadhaa zinazosababisha tatizo la kuwashwa baaada ya kujamiana na mara nyingi tatizo hili huwatokea wanawake mara nyingi kuliko wanaume.
Kwanza kabisa wakati wa kujamiana tuangalie kama tuko wasafi, kwani jasho husababisha muwasho linapoingia ukeni. Mikono yenu wote ni misafi kwani huwezi kukumbuka umeshika nini kabla ya kukutana na mwenzio. Inawezekana ukawa umeshika pilipili na viungo vinavyowasha kama vitunguu na hukunawa vizuri.
Wanawake wanapojisafisha wanashauriwa kwa kutokea mbele kwenda nyuma ili kuepikana kuvutia uchafu wa sehemu ya haja kubwa kwenda ukeni kwani haja kubwa huwa na wadudu wanaoweza kuleta maambukizi ukeni.
Pili kuna mzio (allergy) ya mipira ya kiume au wa kike (Condom), mpira unaweza kuleta muwasho kama ngozi yako ina allergy ya mipira hii. Hii huwatokea baadhi ya wanawake wakati na baada ya kujamiana.
Allergy ya condom husababisha wekundu kwenye uke, kuwashwa na pengine kuvimba. Japo hali hii inaweza kupotea yenyewe baada ya muda mfupi lakini unashauriwa ukiwa nayo umuone daktari kwa ajili ya ushauri.
Allergy nyingine hutokana na mbegu za mwanaume. Kuna aina ya protini inayoweza kumkataa mwenza wako hivyo husababisha muwasho mkali wakati na baada ya kujamiana.
Hii ni mbaya zaidi kwa sababu mwanamke wakati mwingine anaweza kuwashwa mwili mzima na hata kushindwa kupumua vizuri kumuona daktari ili huduma ya haraka itolewe.
Muwasho mwingine unaweza kutokana na magonjwa ya zinaa, miwasho ya magonjwa ya zinaa haitokei mara moja wakati wa kujamiana na pengine inaweza kuchukua saa nyingi na siku kadhaa baada ya kufanya tendo hilo.
Miwasho ya magonjwa ya zinaa inaweza kuambatana na uchafu kutoka ukeni, vipele sehemu za uke na hata wakati mwingine mwanaume anaweza kuumwa tumbola chini ya kitovu.
unashauriwa kumuona daktari ukionadalili hizi mara moja ili kujikinga na maambukizi zaidi. Magonjwa ya ya zinaa yakiwa sugu yanaweza kusababisha ugumba kwa mwanamke hata mwanaume.
Kuna fangasi ambazo hutokea sehemu ya uke na muwasho wake huongezeka pale pindi utakapokutana kimwili na mwanaume, fangasi zinaweza kupona kwa dawa na pia kuzingatia usafi na kuvaa nguo kavu na zilizoanikwa juani au kupigwa pasi.
❎Usiweke nguo za ndani chini ya godoro kwani ni rahisi kuotesha fangasi.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya
pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.
Mzizi Mkavu