Msaada kwa anayejua dawa ya mama mjamzito kutema mate hovyo.

Shindia batuki itasaidia mate kuwa matamu hivyo kukufanya uyameze na kupunguza/kutokua kero kwa waliokaribu nawe kwa kutematema mate
 
Mama vijacho bana, huyo wa kwangu ni hatari..

Hongereni sana kwa kutuletea Watoto wazuri.
 
Dawa ni kujilazimisha kuyameza tu ndani ya siku mbili ,hayata jaa tena mdomoni, ni ngumu ila akiweza na tatizo linakoma, mi ndo ilinisaidia, akijisikia kutema tu, ameze
Nashukuru kwa ushauri amejaribu kutumia njia hii angalau yamepungua japo hayajaisha
 
Tananaona nimezaliwa sijawahi kusikia mama mjamzito anazuiwa kutema hovyo...ngoja akuchukie ndio utakoma hapo kwanini unamkatisha.
Mkuu siyo anazuiliwa kutema mate ila yanamtesa pia anaona aibu kukaa na wenzie sababu muda wote ni kutema mate
 
Kwani kinachosababisha mama mjamzito kutema mate sana ni kipi kitaalamu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…