Msaada kwanini natetemeka sana?

Msaada kwanini natetemeka sana?

Alvin Slain

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
6,375
Reaction score
3,663
Habari wapendwa!

Hili tatizo la kutetemeka wakati ninapowasiliana na wengine sijui litaisha lini.

Maana ni aibu sana nashindwa kuwasilisha hoja zangu makini sababu ya kutetemeka.

Pumzi zinaisha kabisa na nahisi moto unaniwakia ninapotaka kuongea!!
Yaani nashindwa nifanyeje japokua ni suala muhimu kwangu inabidi nikae kimya ili nisijetetemeka"

Nikiongea naona najichanganya sababu ya kupanic!

Kwa anaemjua Dr yoyote wa Saikolojia mjini Arusha naomba mnisaidie na Ushauri pia.
NB:Moderator Paw Invisible
Msiupeleke huu uzi jukwaa la Doktar.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu sifikri kama kuna dawa ya kukufanya usitetemeke ila ni swala la kisaikolojia zaidi nafikiri ukimuona daktari wa saikolojia atakusaidia,hebu jaribu Seliani ile ya mjini acha ile ya Ngaramtoni.

Lakini njia yenyingine kupunguza hilo ni kuelewa kwa ufasaha kile unacho present inapunguza hofu.

Mimi nilikuwa na tatiza hilo mimi liliisha kwa kumuomba Mungu sana maana ilifikia hatua hata nikiongea mbele ya watu 6 natetemeka lakini sasa naongea hata kwa maelfu.
 
Kweli mkuu ni kuomba tu, hiyo ni roho ya hofu. Nami nilikuwa muoga mno ila imeisha kwa maombi tu.
Mkuu sifikri kama kuna dawa ya kukufanya usitetemeke ila ni swala la kisaikolojia zaidi nafikiri ukimuona daktari wa saikolojia atakusaidia,hebu jaribu Seliani ile ya mjini acha ile ya Ngaramtoni.

Lakini njia yenyingine kupunguza hilo ni kuelewa kwa ufasaha kile unacho present inapunguza hofu.

Mimi nilikuwa na tatiza hilo mimi liliisha kwa kumuomba Mungu sana maana ilifikia hatua hata nikiongea mbele ya watu 6 natetemeka lakini sasa naongea hata kwa maelfu.
 
Kweli mkuu ni kuomba tu, hiyo ni roho ya hofu. Nami nilikuwa muoga mno ila imeisha kwa maombi tu.

Mkuu niling`ang`ana na yale maandiko hamkupewa roho yahofu bali ya ujasiri na lile mna ufalme usiotetemeshwa,na kama Roho mt.yuko ndani kwa nini kutetemeka? namtukuza Mungu kwa kweli na wewe hongera sana.
 
Mkuu niling`ang`ana na yale maandiko hamkupewa roho yahofu bali ya ujasiri na lile mna ufalme usiotetemeshwa,na kama Roho mt.yuko ndani kwa nini kutetemeka? namtukuza Mungu kwa kweli na wewe hongera sana.


Hata ninaposoma hizi post nnakua na hofu utadhani watu wananiona
 
Sio utani ni kweli
Vidole vinatetemeka sana ninapomjibu mtu kwenye mitandao hata sms!

labda ungetueleza ni nini hua unaogopa kutoka kwa watu...au hua unawaza nini labda unapoongea na watu kinachokufanya uwe na wasi wasi kihasi hicho..

na pili wazazi wako walikua wakali sana kipindi unakua?
 
labda ungetueleza ni nini hua unaogopa kutoka kwa watu...au hua unawaza nini labda unapoongea na watu kinachokufanya uwe na wasi wasi kihasi hicho..

na pili wazazi wako walikua wakali sana kipindi unakua?


Huwa nnapata wakati mgumu pale ninapoongea halafu watu wote wakawa wananiangalia mimi yaani hii siipendi nahisi kama macho yao yananitoboa.

Kingine sipendi kuangaliwa usoni .
Na nnapoongea sipendi ile hali kama watu hawajaelewa kwa hio wanataka urudie hapo ndio nachanganyikiwa na kupanik pumzi zinaisha mpaka bassss
 
Da ndg pole sana una tatizo km langu, mi niko chuoni yaani cku za presentation kwangu huwa ni balaa, nimeshajaribu kuomba ushauri humu jf lkn pamoja na shauri mbalimbali nzuri lkn tatzo bado linanitafuna.
Wkt mwngne hata lecturer akiwa anafndsha ile anapouliza swali akikuangalia tu hofu na kutetemeka kuna tamalaki hata kitu nakifahamu nakuwa na wasiwasi ajabu, na drs langu tuko wachache kiasi kwamba lazma utaongea tu!
 
Kimsingi tatizo lako ni la kihistoria.
Inawezekana umelelewa na mama wa kambo au walezi/wazazi wakali wenye tabia za kufokea watoto na wasio wapa watoto nafasi ya kujieleza pale wanapokosea.
Jambo hili likakujengea hofo,woga na kutojiamini mpaka hapo ulipofikia.
DAWA/UTATUZI
Anza kwa kutembelea shule ya chekechea imba nao,cheza nao,wape nasaha taratibu ukimaliza makundi ya chekechea unakuja,primary,sekondary,chuo hadi ktk makongamano na warsha.
JISIKIE HURU NAJUA KINACHOKUTESA NI DHANA .
 
Back
Top Bottom